Prof. Ndalichako: Mazingira mazuri ya uwekezaji yamechangia ukuaji wa muko wa NSSF

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Prof. Joyce Ndalichako amesema mazingira mazuri ya uwekezaji yaliyowekwa na Rais, Dk. Samia Suluhu Hassan kwa sekta binafsi yamechochea ukuaji wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Aidha, Prof. Ndalichako amesema ukuaji huo umepelekea thamani ya mfuko kuongezeka pamoja na michango ya wanachama.

Waziri Ndalichako ameyasema hayo Agosti 17, 2023 alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya NSSF kwa mwaka 2022/23 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi wa Maendeleo ya Jamii.

Amesema kwa mwaka 2022 mfuko huo uliandikisha wanachama 233,644 hadi kufikia Juni  mwaka 2023 kulikuwa na wanachama 243,895 na matarajio ifikapo Juni 2024 ni kuwa na wanachama 277,279.

Naye, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Fatuma Toufiq, ameutaka mfuko wa NSSF kuhakikisha unaongeza wanachama zaidi hasa waliopo kwenye sekta isiyo rasmi.

Akijibu hoja za wabunge, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba, amewahakikishia wabunge kuzingatia maoni yao ili kuendelea kuboresha huduma kwa wanachama wake.

spot_img

Latest articles

Sowah, Kante wafungiwa, Aucho naye yumo

Na Winfrida Mtoi NYOTA wa Simba Jonathan Sowah na Allasane Kante wamefungiwa michezo mitano na...

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

More like this

Sowah, Kante wafungiwa, Aucho naye yumo

Na Winfrida Mtoi NYOTA wa Simba Jonathan Sowah na Allasane Kante wamefungiwa michezo mitano na...

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...