Chongolo ‘kuhamia’ Dar

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo, anatarajia kuhutubia katika mkutano wa hadhara utakaofanyika Dar es Salaam Julai 29,2023 katika viwanja vya Tanganyika Pakers Kawe.

Kufanyika kwa mkutano huo ni utekelezaji wa maazimio ya Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa kilichokutana hivi karibuni jijini Dodoma ambacho pamoja na mambo mengine kiliazimia katibu mkuu kufanya mikutano katika mikoa mbalimbali ukiwemo Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Julai 25,2023 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Abasi Mtemvu, amesema katika mkutano huo wataeleza utekekezaji wa Ilani ya Uchaguzi uliofanyika Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi.

“Dhamira ya CCM ni kuendelea kuwaletea wananchi maendeleo, tunawaomba wananchi waje kwa wingi kwenye mkutano huu, tutaeleza utekelezaji wa Ilani na mambo mengi yanayoendelea nchini chini ya usimamizi wa Rais Samia Suluhu Hassan,” amesema Mtemvu.

Chongolo anaendelea na ziara yake katika mikoa mbalimbali nchini ambapo tayari amefanya mikutano Mbeya, Mtwara, Lindi, Singida na Arusha.

spot_img

Latest articles

Msajili wa Hazina aonya taasisi za umma zenye utendaji duni Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeonya taasisi za umma zinazofanya vibaya kujitathmini na kuchukua hatua za...

KAMATI YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI YARIDHISHWA NA MAENDELEO YA UZALISHAJI UMEME KITUO CHA JULIUS NYERERE

📌Yasema Kituo kinachangia asilimia 45 ya umeme katika Gridi ya Taifa 📌Yasisitiza ukamilishaji wa miradi...

MD TWANGE AFAFANUA CHANZO CHA HITILAFU ILIYOTOKEA KWENYE GRIDI YA UMEME YA TAIFA

📌 Aomba radhi kwa wateja wananchi na kuwahakikishia upatikanaji endelevu wa huduma ya umeme 📌...

Hatuna pa kujificha, tuwajibike tu yaishe

TAIFA la Tanzania ni nchi huru iliyojitawala kwa takribani miaka 65 sasa, tangu bendera...

More like this

Msajili wa Hazina aonya taasisi za umma zenye utendaji duni Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeonya taasisi za umma zinazofanya vibaya kujitathmini na kuchukua hatua za...

KAMATI YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI YARIDHISHWA NA MAENDELEO YA UZALISHAJI UMEME KITUO CHA JULIUS NYERERE

📌Yasema Kituo kinachangia asilimia 45 ya umeme katika Gridi ya Taifa 📌Yasisitiza ukamilishaji wa miradi...

MD TWANGE AFAFANUA CHANZO CHA HITILAFU ILIYOTOKEA KWENYE GRIDI YA UMEME YA TAIFA

📌 Aomba radhi kwa wateja wananchi na kuwahakikishia upatikanaji endelevu wa huduma ya umeme 📌...