Chongolo ‘kuhamia’ Dar

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo, anatarajia kuhutubia katika mkutano wa hadhara utakaofanyika Dar es Salaam Julai 29,2023 katika viwanja vya Tanganyika Pakers Kawe.

Kufanyika kwa mkutano huo ni utekelezaji wa maazimio ya Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa kilichokutana hivi karibuni jijini Dodoma ambacho pamoja na mambo mengine kiliazimia katibu mkuu kufanya mikutano katika mikoa mbalimbali ukiwemo Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Julai 25,2023 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Abasi Mtemvu, amesema katika mkutano huo wataeleza utekekezaji wa Ilani ya Uchaguzi uliofanyika Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi.

“Dhamira ya CCM ni kuendelea kuwaletea wananchi maendeleo, tunawaomba wananchi waje kwa wingi kwenye mkutano huu, tutaeleza utekelezaji wa Ilani na mambo mengi yanayoendelea nchini chini ya usimamizi wa Rais Samia Suluhu Hassan,” amesema Mtemvu.

Chongolo anaendelea na ziara yake katika mikoa mbalimbali nchini ambapo tayari amefanya mikutano Mbeya, Mtwara, Lindi, Singida na Arusha.

spot_img

Latest articles

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...

Mradi wa upanuzi Kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Kinyerezi I Extension umekamilika

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema kuwa mradi wa upanuzi...

More like this

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...