Kongamano kuwafunda vijana kiuchumi laja

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Wanafunzi wa vyuo, waendesha bodaboda na makundi mengine ya vijana wanatarajia kupatiwa mafunzo yanayolenga kutambua mchango wao katika kujenga uchumi wa taifa.

Kongamano hilo litakalofanyika Dar es Salaam wakati wa Siku ya Vijana Duniani inayoadhimishwa Agosti 12 kila mwaka limeandaliwa na Shirika lisilokuwa la kiserikali linalojihusisha na uwezeshaji vijana, wanawake, watoto na watu wenye uhitaji maalumu.

Akizungumza na waandishi wa habari Julai 19,2023 Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, Amina Said, amesema wanatambua jitihada zinazofanywa na Serikali ndiyo maana wameweka mikakati ya kuwezesha kundi hilo kwa lengo la kutatua changamoto za ajira zinazolikabili.

“Amo inalenga kumuamsha kijana kujitambua na kujua thamani yake, kijana asipojielewa na kujithamini hata ufanye vipi ni kazi bure.

“Amo inamuamsha kijana aweze kujiongoza mwenyewe na kutimiza malengo yake binafsi,” amesema Amina.

Amesema pia katika kongamano hilo vijana watapata nafasi ya kujifunza mambo mbalimbali kama kujitambua, biashara na uwekezaji, masoko, umuhimu wa kutii sheria na fursa zinazopatikana nchini na kuwataka kuchangamkia fursa hiyo kwa kujisajili.

Mkurugenzi huyo amesema watawawezesha vijana kwa kuwapatia vitendea kazi kama vile bodaboda, vyerehani, mitungi ya gesi na majiko yake.

Naye Mwalimu wa Saikolojia katika shirika hilo, Neema Bachu, amesema wataanza Dar es Salaam kisha kwenda katika mikoa mbalimbali kwa sababu tayari wamepokea maombi ya kuwafikia vijana.

Mgeni rasmi katika kongamano hilo lenye kaulimbiu isemayo ‘Uwajibikaji wetu ndio uhai wa uchumi wetu’ anatarajiwa kuwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Patrobas Katambi.

spot_img

Latest articles

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

Dk. Nchimbi: Serikali imejipanga kuimarisha sekta ya uchukuzi

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi amesema serikali imejizatiti kuhakikisha...

More like this

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...