Kongamano kuwafunda vijana kiuchumi laja

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Wanafunzi wa vyuo, waendesha bodaboda na makundi mengine ya vijana wanatarajia kupatiwa mafunzo yanayolenga kutambua mchango wao katika kujenga uchumi wa taifa.

Kongamano hilo litakalofanyika Dar es Salaam wakati wa Siku ya Vijana Duniani inayoadhimishwa Agosti 12 kila mwaka limeandaliwa na Shirika lisilokuwa la kiserikali linalojihusisha na uwezeshaji vijana, wanawake, watoto na watu wenye uhitaji maalumu.

Akizungumza na waandishi wa habari Julai 19,2023 Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, Amina Said, amesema wanatambua jitihada zinazofanywa na Serikali ndiyo maana wameweka mikakati ya kuwezesha kundi hilo kwa lengo la kutatua changamoto za ajira zinazolikabili.

“Amo inalenga kumuamsha kijana kujitambua na kujua thamani yake, kijana asipojielewa na kujithamini hata ufanye vipi ni kazi bure.

“Amo inamuamsha kijana aweze kujiongoza mwenyewe na kutimiza malengo yake binafsi,” amesema Amina.

Amesema pia katika kongamano hilo vijana watapata nafasi ya kujifunza mambo mbalimbali kama kujitambua, biashara na uwekezaji, masoko, umuhimu wa kutii sheria na fursa zinazopatikana nchini na kuwataka kuchangamkia fursa hiyo kwa kujisajili.

Mkurugenzi huyo amesema watawawezesha vijana kwa kuwapatia vitendea kazi kama vile bodaboda, vyerehani, mitungi ya gesi na majiko yake.

Naye Mwalimu wa Saikolojia katika shirika hilo, Neema Bachu, amesema wataanza Dar es Salaam kisha kwenda katika mikoa mbalimbali kwa sababu tayari wamepokea maombi ya kuwafikia vijana.

Mgeni rasmi katika kongamano hilo lenye kaulimbiu isemayo ‘Uwajibikaji wetu ndio uhai wa uchumi wetu’ anatarajiwa kuwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Patrobas Katambi.

spot_img

Latest articles

Wanawake TRA Wapongezwa kwa Mchango wa Ukusanyaji Mapato

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu Mwamba, amewapongeza wanawake wa...

Mchungaji Kimaro: Miradi ya Familia Ndio Suluhisho la Ajira kwa Vijana

Na Mwandishi Wetu  MCHUNGAJI wa Kanisa la Kiinjiri Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kijitonyama Dk....

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani: TRA Yakabidhi Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Milioni 40

Na Tatu Mohamed KUELEKEA maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8,...

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

More like this

Wanawake TRA Wapongezwa kwa Mchango wa Ukusanyaji Mapato

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu Mwamba, amewapongeza wanawake wa...

Mchungaji Kimaro: Miradi ya Familia Ndio Suluhisho la Ajira kwa Vijana

Na Mwandishi Wetu  MCHUNGAJI wa Kanisa la Kiinjiri Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kijitonyama Dk....

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani: TRA Yakabidhi Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Milioni 40

Na Tatu Mohamed KUELEKEA maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8,...