Kongamano kuwafunda vijana kiuchumi laja

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Wanafunzi wa vyuo, waendesha bodaboda na makundi mengine ya vijana wanatarajia kupatiwa mafunzo yanayolenga kutambua mchango wao katika kujenga uchumi wa taifa.

Kongamano hilo litakalofanyika Dar es Salaam wakati wa Siku ya Vijana Duniani inayoadhimishwa Agosti 12 kila mwaka limeandaliwa na Shirika lisilokuwa la kiserikali linalojihusisha na uwezeshaji vijana, wanawake, watoto na watu wenye uhitaji maalumu.

Akizungumza na waandishi wa habari Julai 19,2023 Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, Amina Said, amesema wanatambua jitihada zinazofanywa na Serikali ndiyo maana wameweka mikakati ya kuwezesha kundi hilo kwa lengo la kutatua changamoto za ajira zinazolikabili.

“Amo inalenga kumuamsha kijana kujitambua na kujua thamani yake, kijana asipojielewa na kujithamini hata ufanye vipi ni kazi bure.

“Amo inamuamsha kijana aweze kujiongoza mwenyewe na kutimiza malengo yake binafsi,” amesema Amina.

Amesema pia katika kongamano hilo vijana watapata nafasi ya kujifunza mambo mbalimbali kama kujitambua, biashara na uwekezaji, masoko, umuhimu wa kutii sheria na fursa zinazopatikana nchini na kuwataka kuchangamkia fursa hiyo kwa kujisajili.

Mkurugenzi huyo amesema watawawezesha vijana kwa kuwapatia vitendea kazi kama vile bodaboda, vyerehani, mitungi ya gesi na majiko yake.

Naye Mwalimu wa Saikolojia katika shirika hilo, Neema Bachu, amesema wataanza Dar es Salaam kisha kwenda katika mikoa mbalimbali kwa sababu tayari wamepokea maombi ya kuwafikia vijana.

Mgeni rasmi katika kongamano hilo lenye kaulimbiu isemayo ‘Uwajibikaji wetu ndio uhai wa uchumi wetu’ anatarajiwa kuwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Patrobas Katambi.

spot_img

Latest articles

IAEA yaipongeza Zanzibar kwa Ushirikiano Katika Kilimo na Mifugo

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Suleiman Masoud Makame,...

Wakurugenzi Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa kwa siku tano

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) kwa kushirikiana na Taasisi ya...

Mkurugenzi Mkuu NIRC atoa pole kwa waandishi wa habari waliopata ajali Iringa

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Raymond Mndolwa,...

Baraza la wafanyakazi Siri ya utendaji bora

Na Mwandishi Wetu BARAZA la Wafanyakazi la Sita la TMDA limefanyika kwa ufanisi tarehe...

More like this

IAEA yaipongeza Zanzibar kwa Ushirikiano Katika Kilimo na Mifugo

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Suleiman Masoud Makame,...

Wakurugenzi Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa kwa siku tano

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) kwa kushirikiana na Taasisi ya...

Mkurugenzi Mkuu NIRC atoa pole kwa waandishi wa habari waliopata ajali Iringa

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Raymond Mndolwa,...