CRDB yajipanga kuwezesha wabunifu Kibiashara

Na Mwandishi Wetu 

BENKI ya CRDB imesema ipo tayari kuunga mkono tasnia ya ubunifu nchini kwa kuweka mifumo ya kifedha itakayowawezesha wabunifu kubadili vipaji vyao na kuwa biashara endelevu zenye mchango wa moja kwa moja katika uchumi wa Taifa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa Jukwaa la Mitindo Tanzania, Meneja wa Huduma kwa Wateja Wadogo na wa Kati kutoka Benki ya CRDB, Japhary Hassanal, amesema kuunganisha ubunifu na mifumo ya biashara ni hatua muhimu katika kuimarisha mchango wa sekta hiyo katika maendeleo ya nchi.

“Lengo letu ni kuona ubunifu uliopo unageuzwa kuwa biashara zenye tija, ajira na mchango halisi katika uchumi wa Taifa,” amesema Japhary.

Ameeleza kuwa CRDB inatambua nafasi ya sekta ya mitindo katika kukuza biashara ndogo na za kati, ajira kwa vijana na wanawake pamoja na kupanua wigo wa uchumi wa ubunifu nchini.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wabunifu Tanzania (FAT), Mustafa Hassanal, amesema tasnia ya mitindo ina uwezo mkubwa wa kuchochea uchumi kupitia viwanda, biashara na diplomasia ya kiuchumi endapo itawekewa mifumo imara na sera rafiki.

“Mitindo leo si suala la urembo pekee, bali ni sekta ya kimkakati inayogusa ajira, biashara na utambulisho wa Taifa,” amesema Hassanal.

Ameongeza kuwa kwa muda mrefu mitindo barani Afrika imekuwa ikionekana kama kipaji kisicho na mifumo madhubuti ya kifedha na kibiashara, hali iliyodhoofisha ukuaji wa sekta hiyo licha ya kuwepo kwa vipaji vingi.

Hassanal amesema Jukwaa la Mitindo Tanzania limeanzishwa ili kuwakutanisha wadau mbalimbali kwa lengo la kujadili changamoto na kuweka mikakati ya vitendo ya kuigeuza mitindo kutoka kipaji binafsi na kuwa sekta rasmi ya uchumi wa Taifa.

spot_img

Latest articles

Serikali yatoa maelekezo nane kuimarisha kampuni ambazo ina umiliki hisa chache kuelekea Dira 2050

Na Mwandishi wetu, Arusha SERIKALI imetoa maelekezo nane ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa kampuni...

Uwekezaji wa Shilingi Bilioni 50 Kituo Cha Mpomvu waimarisha upatikanaji wa umeme Kanda ya Ziwa

📌 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yakagua Kituo cha Kupokea...

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

CRDB YAZINDUA KAMPENI YA ‘FAINALI NDIO MPANGO NA TEMBOCARD VISA’

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imezindua kampeni yake mpya ya 'Fainali ndio Mpango...

More like this

Serikali yatoa maelekezo nane kuimarisha kampuni ambazo ina umiliki hisa chache kuelekea Dira 2050

Na Mwandishi wetu, Arusha SERIKALI imetoa maelekezo nane ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa kampuni...

Uwekezaji wa Shilingi Bilioni 50 Kituo Cha Mpomvu waimarisha upatikanaji wa umeme Kanda ya Ziwa

📌 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yakagua Kituo cha Kupokea...

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...