Waziri Aweso aweka kambi Dar kupambana na changamoto upungufu wa maji

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso (Mb) amefanya ziara ya kikazi katika Mkoa wa Dar es salaam na Pwani kwa kutembelea matanki makubwa ya uhifadhi Maji, mtambo wa uzalishaji maji wa Ruvu Chini ili kujionea hali ilivyo ya uzalishaji maji na usambazaji Ikiwa ni mwendelezo wa jitihada za Wizara ya Maji kupunguza changamoto ya upungufu wa Maji uliojitokeza kutokana na kuchelewa kwa mvua.

Waziri Aweso amewasihi Wananchi kujenga utamaduni wa kuwa na vyombo vya kutunza na kuhifadhi maji katika kipindi hiki na ameitaka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) kushirikiana na wadau binafsi wenye visima vikubwa ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma.

Pia Waziri Aweso ameongeza kwa kutoa maagizo kwa DAWASA kuhakikisha visima vyote vilivyochimbwa na Serikali vinaingizwa kwenye mfumo wa usambazaji ili kuongeza upatikanaji wa maji kwa Wananchi.

spot_img

Latest articles

Mnyama Simba afia kwa Mkapa, Yanga, Azam kicheko

Na Winfrida Mtoi LIGI Kuu Tanzania Bara imeendelea leo Novemba 7, 2025 kwa michezo miwili...

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

More like this

Mnyama Simba afia kwa Mkapa, Yanga, Azam kicheko

Na Winfrida Mtoi LIGI Kuu Tanzania Bara imeendelea leo Novemba 7, 2025 kwa michezo miwili...

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...