Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu  ajiuzulu TEF

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari Machumu amejiuzulu nafasi ya makamu mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF).

Machumu amekabidhi barua ya kujiuzulu kwake kwa Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile, leo Jumatano Novemba 26, 2025 alipokutana na wahariri kwenye kikao cha ndani, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Amesema kwa nafasi yake mpya anaona kutakuwa na mgongano wa masilahi na wadhifa huo.

Baada ya kupokea barua hiyo, Balile amekubali kujiuzulu kwa Machumu na kuwa Kamati ya Utendaji ya TEF itakaa baadaye leo kujadili suala hilo.

Machumu aliteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan hivi karibuni kuwa mkurugenzi wa mawasiliano ya Rais Ikulu.

spot_img

Latest articles

CRDB yajipanga kuwezesha wabunifu Kibiashara

Na Mwandishi Wetu  BENKI ya CRDB imesema ipo tayari kuunga mkono tasnia ya ubunifu nchini...

MAB yateta na wadhibiti Mutukula OSBP

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI Bodi ya Ushauri ya Wizara kwa TMDA (MAB), Eric Shitindi...

Rais Samia: Hakuna mtoto atafika darasa la tatu bila kujua kusoma, kuandika na kuhesabu

Na Tatu Mohamed RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan,...

More like this

CRDB yajipanga kuwezesha wabunifu Kibiashara

Na Mwandishi Wetu  BENKI ya CRDB imesema ipo tayari kuunga mkono tasnia ya ubunifu nchini...

MAB yateta na wadhibiti Mutukula OSBP

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI Bodi ya Ushauri ya Wizara kwa TMDA (MAB), Eric Shitindi...