Watuhumiwa 57 wa uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu

Mahakama ya Wilaya ya Ilemela imewaachia huru watuhumiwa 57 kati 61 wa kesi ya uhaini waliokuwa wakishikiliwa kufuatia  maandamano na matukio ya vurugu za baada ya uchaguzi yalitokea kuanzia Oktoba 29, 2025.

Uamuzi wa kufuta mashtaka hayo umetolewa leo Novemba 24,2025 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Stella Kiama, katika Mahakama ya Wilaya ya Ilemela iliyopo kwenye Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki, Buswelu.

Hatua hiyo imetokana na  upande wa mashtaka, kupitia Wakili wa Serikali Mwandamizi, Safi Amani, kuwasilisha ombi la Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) la kutokuwa na nia ya kuendelea na mashtaka dhidi ya watuhumiwa hao waliokuwa wanakabiliwa na tuhuma mbalimbali.

Shauri hilo namba 26641/2025 limeletwa kwa ajili ya kutajwa kwa mara ya pili mahakamani hapo leo ambapo kwa mara ya kwanza lilitajwa Novemba 24, 2025.

Vijana hao ni miongoni mwa wale waliokuwa wamekamatwa na Jeshi la Polisi na baadaye kufikishwa Mahakamani wakidaiwa kuhusika kwa namna moja au nyingine kwenye maandamano yaliyozaa vurugu zilizopelekea uharibifu wa mali, majeruhi na vifo.

spot_img

Latest articles

TTB yaeleza Utalii wa michezo unavyochangia uchumi wa jamii

Na Mwandishi Wetu, Njombe BODI ya Utalii Tanzania (TTB), imesema utalii wa...

Tume Jaji Chande imekwepa kututajia aliyekutwa na ngozi ya ng’ombe

NINGALI ninaitafakari ripoti ya Jaji Mohammed Chande ya matukio ya Oktoba 2025 wakati na...

Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na...

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...

More like this

TTB yaeleza Utalii wa michezo unavyochangia uchumi wa jamii

Na Mwandishi Wetu, Njombe BODI ya Utalii Tanzania (TTB), imesema utalii wa...

Tume Jaji Chande imekwepa kututajia aliyekutwa na ngozi ya ng’ombe

NINGALI ninaitafakari ripoti ya Jaji Mohammed Chande ya matukio ya Oktoba 2025 wakati na...

Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na...