Mwigulu Waziri Mkuu wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limemthibitisha Dk. Mwigulu Nchemba, kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania akichukua nafasi ya Kassim Majaliwa.

Mwigulu amethibitishwa  leo Novemba 13, 2025  kwa kura za ndio 369 kati ya kura 371 zilizopigwa huku za hapana hakuna na  zilizoharibika zikiwa ni mbili.

Uthibitisho huo wa Bunge ni baada ya  Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kumteua Mwigulu ambaye ni Mbunge wa Iramba Magharibi, Mkoani Singida, pia alikuwa Waziri wa Fedha katika kipindi kilichopita.

Akitoa hotuba ya shukrani baada ya kuidhinishwa bungeni jijini Dodoma, Waziri huyo mteule, , amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoingia katika awamu yake ya pili ina kazi kubwa ya kusimamia utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025–2050, ambayo inalenga kuleta mafanikio makubwa ya kiuchumi na kijamii nchini.

Amesema Dira hiyo inaweka kipaumbele kwenye masuala ya ajira, ambapo lengo ni kutoa ajira milioni nane kwa vijana nchini.

Ameeleza kuwa  anatambua changamoto ya ajira kwa vijana na ameahidi kushirikiana kwa karibu na Rais Samia Suluhu Hassan kuhakikisha ajira zinapatikana na umasikini unaokadiriwa kufikia asilimia 26 unapungua kwa kiwango kikubwa.

spot_img

Latest articles

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...

Zungu achaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu MBUNGE mteule wa Jimbo la Ilala Mussa Azzan Zungu ameibuka mshindi...

More like this

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...