Heche akamatwa na Polisi Dar, apelekwa Tarime

Na Mwandishi Wetu

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)Tanzania Bara, John Heche, amekamatwa na Polisi wakati akiingia Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam na kusafirishwa kwenda Tarime.

Katibu Mkuu wa Chadema John Mnyika amesema kiongozi huyo alikuwa anakwenda mahakamani kwa ajili ya kusikiliza kesi ya Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu inayoendelea.

Akizungumzia sababu za kukamatwa kwa Heche, mbeleza na waandishi wa habari leo Oktoba 22,2025, Mkurugenzi wa Sheria na Haki za Binadamu wa Chadema, Wakili Gaston Garubindi amesema wamefuatilia na kuambiwa na Jeshi la Polisi kuwa jambo la Heche   halipo Dar es Salaam lipo Tarime na wamedai kuwa  tayari wameshamsafirisha kuelekea huko.

“Taarifa ya Jeshi la Polisi wanadai ni kweli wamemkamata John Heche, kwa makossa ambayo hawajayasema, lakini anasema jambo lake lipo Tarime na kwamba  tuhuma zake zipo kule na tayari  wamemsafirisha kutoka Dar es Salaam kwenda Tarime.

“Kama Chama tunajipanga sasa kwa maana ya kuagiza mawakili waliopo Mkoa wa Mara na wengine kutoka Mwanza  ili  waelekee huko ili kutoa huduma ya Kisheria kwa Makamu Mwenyekiti,” amesema Wakili Garubindi.

Amesema Heche alikuwa hajapewa wito wowote wa kuitwa Polisi, hivyo wanasubiria atakapofikishwa hule watajua tuhuma zake ni nini.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...