Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Matha Japheth (44), kabila ni Mnyamwezi , Mkulima Mkazi wa Kitongoji cha Mzalendo Kijiji cha Mawemeru , Kata ya Nyarugusu Wilaya ya Geita kwa tuhuma za kumuuwa mume wake na kumfukia katika shimo ndani nyumba yao.

Kwa mujibu wa  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Safia Jongo taarifa ya awali inaeleza chanzo ni mgogoro wa kifamilia baina ya mke na mume ambaye kwa sasa ni marehemu.

“Baada ya mahojiano makali mwanamke huyu alikiri kwamba marehemu ni mume wake na kwamba siku hiyo ya tarehe 11 majira ya usiku mwanaume alirudi nyumbani lakini wakawa na ugomvi ambao ulisababisha kumshambulia kwa kitu chenye ncha kali na baada ya kumshambulia mwanaume huyo alifariki dunia na baada ya hapo akaamua kuchimba shimo ndani ya nyumba yao na kisha kumfukia,“ amesema  Kamanda Safia.

spot_img

Latest articles

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

More like this

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...