Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo Kuu la Songea, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT) – Mwanza, aliyeripotiwa kupotea mnamo Oktoba 09, 2025.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 17,2025  Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Marco  Chilya, amesema Padre huyo hakutekwa kama ambavyo ilidhaniwa bali alijipoteza kutokana na sababu za msongo wa mawazo.

Kamanda huyo ameeleza kuwa Padre amepatikana akiwa hai katika mashamba ya Kijiji cha Mawa, kilichopo Kata ya Hanga, Wilaya ya Namtumbo ambapo ni nyumbani kwao.

Aidha ameongeza kuwa Padre huyo alikutwa akiwa  amedhoofika kwa njaa huku akiwa na begi dogo la mgongoni ambalo lilikuwa na taulo alilokuwa akitumia kulalia, hati yake ya kusafiria, karanga alizokuwa akitumia kama chakula, maji, funguo ya chumba alichokuwa akitumia kabla ya jimboni kwake, fedha taslimu kiasi cha Shilingi 13,500, saa ya mkononi, simu ya mkononi akiwa ameizima  pamoja na dawa za  maumivu.

Ameeleza kuwa  kwa sasa Padre huyo amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songea (Homso) akiendelea na matibabu kutokana na kudhoofika kwa afya yake.

spot_img

Latest articles

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...

More like this

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...