EWURA yatoa rai kuhusu vibali vya ujenzi wa Vituo vya Mafuta

Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetoa rai kwa wafanyabiashara wanaokusudia kuanzisha vituo vya mafuta kuhakikisha wanapata kibali cha ujenzi kutoka EWURA kabla ya kuanza ujenzi.

Rai hiyo imetolewa leo tarehe 3 Oktoba 2025, mkoani Iringa na Meneja wa Kanda ya Kati wa EWURA, Hawa Lweno, wakati wa mkutano na wadau wa sekta ndogo za mafuta, umeme na maji.

Lweno amesema kumekuwa na mwitikio mkubwa wa wafanyabiashara kufungua vituo vya mafuta hasa maeneo ya vijijini, lakini changamoto imeibuka pale ambapo baadhi yao huanza ujenzi bila kuwa na kibali cha EWURA.

“Natoa wito kwa yeyote mwenye nia ya kuanzisha kituo cha mafuta kuhakikisha kwanza anapata kibali kutoka EWURA kabla ya kuanza ujenzi. Kukiuka sharti hili la kisheria kutasababisha mfanyabiashara husika kutozwa faini ya shilingi milioni 20,” amesema.

Kibali hicho ni muhimu kwa kuwa kinatoa nafasi kwa wataalamu wa EWURA kuhakiki na kujiridhisha kwamba ujenzi wa kituo husika unazingatia viwango na masharti ya kiafya, kiusalama na kimazingira yaliyowekwa.

Kwa upande wake, mmoja wa washiriki wa mkutano huo, David Mlyapatali, amesema kikao hicho kimekuwa na manufaa makubwa kwani kimewapa uelewa zaidi kuhusu taratibu na wajibu wao katika kuendesha biashara hizo.

spot_img

Latest articles

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...

Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo...

Waangalizi wa Uchaguzi watakiwa kutoingilia mchakato wa Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi wetu, Dodoma WAANGALIZI wa Uchaguzi wa ndani na wa kimataifa wametakiwa kuzingatia sheria...

More like this

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...

Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo...

Waangalizi wa Uchaguzi watakiwa kutoingilia mchakato wa Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi wetu, Dodoma WAANGALIZI wa Uchaguzi wa ndani na wa kimataifa wametakiwa kuzingatia sheria...