Bei za Petroli, Dizeli zaendelea kushuka

Na Mwandishi Wetu

BEI ya mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa kwa mwezi Oktoba 2025 zimeendelea kushuka ambapo bei za rejareja za petroli zimepungua kwa sh. 55, dizeli sh 50 ikiwa ni muendelezo wa kupungua kwa bei za bidhaa hizo .

Kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Dkt. James Mwainyekule, kupungua kwa bei hizo kumetokana na kupungua kwa gharama za kubadilisha fedha za kigeni kwa wastani wa 5.10% huku gharama za kuagiza mafuta ya petroli kwa bandari ya Dar es Salaam zikipungua kwa wastani wa 1.95% .

Taarifa hiyo imeeleza kuwa, mafuta yaliyopokelewa bandari ya Dar es Salaam, imepungua kutoka sh 2,807 hadi 2,752 kwa petroli, na kutoka sh. 2,754 hadi sh. 2,704 kwa dizeli huku bei ya mafuta ya taa ikisalia kuwa sh. 2,774 kama ilivyokuwa Septemba 2025.

Mafuta ya petroli yaliyopokelewa katika Bandari ya Tanga, bei ya rejareja nayo imepungua kutoka sh. 2,868 hadi sh. 2,813, dizeli kutoka sh 2,816 hadi sh. 2, 766 na bei ya mafuta ya taa ikisalia kuwa sh. 2,835 kama ilivyokuwa kwa mwezi uliopita.

Kwa upande wa mafuta yanayopokelewa Bandari ya Mtwara, bei ya petroli imepungua kutoka sh. 2,899 hadi sh. 2,844, na dizeli kutoka Sh. 2,847 hadi 2,797 huku bei ya mafuta ya taa ikisalia sh 2, 866 kama ilivyokuwa Septemba 2025.

spot_img

Latest articles

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

Serikali yaahidi kuimarisha uwezeshaji wa Makundi Maalum kupitia ajenda ya Maendeleo Jumuishi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt....

More like this

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...