Bei za Petroli, Dizeli zaendelea kushuka

Na Mwandishi Wetu

BEI ya mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa kwa mwezi Oktoba 2025 zimeendelea kushuka ambapo bei za rejareja za petroli zimepungua kwa sh. 55, dizeli sh 50 ikiwa ni muendelezo wa kupungua kwa bei za bidhaa hizo .

Kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Dkt. James Mwainyekule, kupungua kwa bei hizo kumetokana na kupungua kwa gharama za kubadilisha fedha za kigeni kwa wastani wa 5.10% huku gharama za kuagiza mafuta ya petroli kwa bandari ya Dar es Salaam zikipungua kwa wastani wa 1.95% .

Taarifa hiyo imeeleza kuwa, mafuta yaliyopokelewa bandari ya Dar es Salaam, imepungua kutoka sh 2,807 hadi 2,752 kwa petroli, na kutoka sh. 2,754 hadi sh. 2,704 kwa dizeli huku bei ya mafuta ya taa ikisalia kuwa sh. 2,774 kama ilivyokuwa Septemba 2025.

Mafuta ya petroli yaliyopokelewa katika Bandari ya Tanga, bei ya rejareja nayo imepungua kutoka sh. 2,868 hadi sh. 2,813, dizeli kutoka sh 2,816 hadi sh. 2, 766 na bei ya mafuta ya taa ikisalia kuwa sh. 2,835 kama ilivyokuwa kwa mwezi uliopita.

Kwa upande wa mafuta yanayopokelewa Bandari ya Mtwara, bei ya petroli imepungua kutoka sh. 2,899 hadi sh. 2,844, na dizeli kutoka Sh. 2,847 hadi 2,797 huku bei ya mafuta ya taa ikisalia sh 2, 866 kama ilivyokuwa Septemba 2025.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...