THBUB yawaasa waandishi wa habari kuelekea uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu

TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), imewaasa waandishi wa habari nchini, kujiepusha kuchapisha, kutangaza habari zenye lengo la kuchochea vurugu, ubaguzi, chuki za kisiasa, kikabila, kidini na jinsi.

Hayo yamesemwa na Katibu Mtendaji wa THBUB, Patience Ntwina,, wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari yaliyofanyika leo Jumatatu Septemba 22, 2025 katika Ukumbi wa Tume hiyo, Luthul, Dar es Salaam.

Katika mafunzo hayo yaliyoandaliwa kuhusu Haki za Binadamu na Wajibu wa Waandishi wa Habari wakati wa uchaguzi, Ntwina, alisema kipindi cha kupiga kura katika Uchaguzi MKuu wa Urais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu, waandishi wa habari wanatakiwa kuepuka kufanya kampeni kwa namna yoyote.

Nkwina alisema siku ya kupiga kura haitakiwi kuvaa mavazi yenye alama ya chama au mgombea fulani. Ametoa with kwa waandishi wa habari kuchukua tahadhari dhidi ya matumizi ya mabaya ya majukwaa ya habari ikiwamo mitandao ya kijamii.

Pia amevitaka vyombo vya habari kujikita katika kuimarisha amani, utulivu na demokrasia nchini kwa kutotumika vibaya kalamu zao.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...