Watumishi Wizara ya Nishati wapatiwa elimu ya matumizi sahihi ya Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu

WATUMISHI wa Wizara ya Nishati leo wamepata elimu ya matumizi bora na sahihi ya majiko yanayotumia umeme kidogo ( Induction cookers) baada ya kukabidhiwa majiko hayo na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko hivi karibuni.

Dkt. Biteko aliwakabidhi majiko hayo Watumishi wa Wizara ya Nishati ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia na kwa kutambua kuwa Watumishi hao ni mabalozi katika utoaji wa elimu ya Nishati Safi ya Kupikia kwa wananchi.

Mafunzo hayo ambayo yamefanyika katika Ofisi za Wizara ya Nishati- Mtumba, Dodoma yameandaliwa na Kitengo cha Nishati safi ya kupikia kwa kushirikiana na wataalam kutoka Kampuni ya Positive Cooker.

Akitoa elimu ya matumizi bora na sahihi ya majiko hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Positive Cooker, Atukuzwe Willson ameeleza kuwa lengo la utoaji wa mafunzo hayo ni sehemu ya uhamasishaji wananchi kutumia umeme kwa matumizi ya kupikia kupitia majiko janja yanayotumia umeme kidogo.

“Lengo la kutoa elimu hii ni kuhakikisha kila Mtanzania anaachana na matumizi ya nishati isiyosafi ili kulinda mazingira pamoja na afya zetu lakini pia ni sehemu ya jitihada za kuunga mkono kampeni ya nishati safi ya kupikia ambapo hadi kufikia mwaka 2034 asilimia 80 ya watanzania wanapaswa kutumia nishati safi ya kupikia,” amesema Willson.

Akizungumza kuhusu majiko hayo janja ya umeme amesema yanatumia wastani wa nusu uniti hadi uniti moja na nusu kwa wastani wa dakika 15 mpaka dakika 90 sawa na shilingi 65 mpaka shilingi 534 tu hali inayothibitisha ufanisi wa majiko hayo kuwa na gharama nafuu, kuokoa muda, kulinda afya pamoja na mazingira.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...