Mpina ashinda kesi, ruksa kugombea Urais

Na Mwandishi Wetu

Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Luhaga Mpina leo Septemba 11, 2025 ameshinda kesi ya kupinga kuzuiwa kurejesha fomu za uteuzi wa mgombea Urais aliyofunguliwa dhidi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na mahakama kuamuru taratibu ziendelee zilipoishia.

Kesi hiyo namba 21692/2025, iliyofunguliwa na Bodi ya Wadhamini wa ACT Wazalendo pamoja na Lugaha Mpina, ikipinga uamuzi wa INEC kumuengua mgombea wao wa Urais, katika orodha ya wagombea.

Jopo la majaji watatu, Abdi Kagomba, Evaristo Longopa na John Kahyoza ndiyo waliokuwa wakisikiliza kesi hiyo. Majaji hao wamesema INEC ni Tume huru na haikupaswa kusikiliza maelekezo ya mtu au taasisi yoyote.


Mahakama imesema kitendo cha INEC kutopokea fomu za Mpina, ilimnyima haki ya kikatiba na ya kusikilizwa, hivyo kuamuru impe fursa mgombea huyo kuwasilisha fomu zake na mchakato uendelee ulipoishia.

INEC ilichukua uamuzi  huo, kutokana na taarifa ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, aliyobainisha kuwa Mpina hakutimiza vigezo vya uanachama kwa mujibu wa kanuni za chama, pia kutokana na  malalamiko ya kada wa chama hicho, Monalisa Ndala aliyedai kuwa mkutano mkuu  uliompitisha Mpina haukufuata katiba.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...