Mpina ashinda kesi, ruksa kugombea Urais

Na Mwandishi Wetu

Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Luhaga Mpina leo Septemba 11, 2025 ameshinda kesi ya kupinga kuzuiwa kurejesha fomu za uteuzi wa mgombea Urais aliyofunguliwa dhidi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na mahakama kuamuru taratibu ziendelee zilipoishia.

Kesi hiyo namba 21692/2025, iliyofunguliwa na Bodi ya Wadhamini wa ACT Wazalendo pamoja na Lugaha Mpina, ikipinga uamuzi wa INEC kumuengua mgombea wao wa Urais, katika orodha ya wagombea.

Jopo la majaji watatu, Abdi Kagomba, Evaristo Longopa na John Kahyoza ndiyo waliokuwa wakisikiliza kesi hiyo. Majaji hao wamesema INEC ni Tume huru na haikupaswa kusikiliza maelekezo ya mtu au taasisi yoyote.


Mahakama imesema kitendo cha INEC kutopokea fomu za Mpina, ilimnyima haki ya kikatiba na ya kusikilizwa, hivyo kuamuru impe fursa mgombea huyo kuwasilisha fomu zake na mchakato uendelee ulipoishia.

INEC ilichukua uamuzi  huo, kutokana na taarifa ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, aliyobainisha kuwa Mpina hakutimiza vigezo vya uanachama kwa mujibu wa kanuni za chama, pia kutokana na  malalamiko ya kada wa chama hicho, Monalisa Ndala aliyedai kuwa mkutano mkuu  uliompitisha Mpina haukufuata katiba.

spot_img

Latest articles

Mvua za vuli kunyesha kwa wastani  kuanzia  Oktoba

Na Mwandishi Wetu Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetangaza kuwa msimu wa mvua...

Tembo Warriors yatinga nusu fainali CECAAF

Na Mwandishi Wetu Timu ya Taifa ya watu wenye ulemavu Tanzania 'Tembo Warriors' imefanikiwa kutinga...

Ajali yaua wanafunzi wawili wa kidato cha sita

Na Mwandishi Wetu Watu saba wamefariki dunia wakiwamo wanafunzi wawili wa kidato cha sita shule...

Mahakama kuamua hatma ya Lissu Jumatatu

Na Mwandishi Wetu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa, Tundu Lissu,  amerejeshwa...

More like this

Mvua za vuli kunyesha kwa wastani  kuanzia  Oktoba

Na Mwandishi Wetu Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetangaza kuwa msimu wa mvua...

Tembo Warriors yatinga nusu fainali CECAAF

Na Mwandishi Wetu Timu ya Taifa ya watu wenye ulemavu Tanzania 'Tembo Warriors' imefanikiwa kutinga...

Ajali yaua wanafunzi wawili wa kidato cha sita

Na Mwandishi Wetu Watu saba wamefariki dunia wakiwamo wanafunzi wawili wa kidato cha sita shule...