Mahakama kuamua hatma ya Lissu Jumatatu

Na Mwandishi Wetu

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa, Tundu Lissu,  amerejeshwa mahabusu leo na anatarajiwa kurejea  Jumatatu Septemba 15, 2025 kwa ajili ya Mahakama  kutoa uamuzi juu ya mapingamizi aliyowasilisha kuhusu kesi ya uhaini inayomkabili.

Kesi hiyo imesikilizwa  siku nne mfululizo tangu Jumatatu katika Mahakam Kuu ya Tanzania Masjala ndogo ya Dar es Salaam mbele ya jopo la Majaji watatu, wakiongozwa na Jaji Dustan Nduguru akisaidiana na Jaji James Karayemaha na Ferdinand Kiwonde.

Tayari Lissu amekamilisha mawasilisho ya mapingamizi yake leo Septemba 11, 2025, madai ya msingi ikiwa ni mchakato wa kesi hiyo katika Mahakama ya Kisutu ulikuwa na makosa mengi na kutaka kesi ifutwe, aachiwe huru, hivyo kinachosubiriwa ni uamuzi kutoka kwa jopo la Majaji watatu.

Iwapo Mahakama Kuu itakubaliana na hoja za Lissu, kesi hiyo inaweza kufutwa rasmi, endapo hoja zikikataliwa basi itaendelea kusikilizwa kwa mujibu wa taratibu za kisheria.

Akizungumza na waandishi wa habari nje ya mahakama hiyo, Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika amesema wakati dunia itakuwa inaadhimisha Siku ya Demokrasia, kwao itakuwa tofauti kwani watakuwa mahakamani kujua hatma ya kesi ya Mwenyekiti wao.

spot_img

Latest articles

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

More like this

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...