Mahakama kuamua hatma ya Lissu Jumatatu

Na Mwandishi Wetu

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa, Tundu Lissu,  amerejeshwa mahabusu leo na anatarajiwa kurejea  Jumatatu Septemba 15, 2025 kwa ajili ya Mahakama  kutoa uamuzi juu ya mapingamizi aliyowasilisha kuhusu kesi ya uhaini inayomkabili.

Kesi hiyo imesikilizwa  siku nne mfululizo tangu Jumatatu katika Mahakam Kuu ya Tanzania Masjala ndogo ya Dar es Salaam mbele ya jopo la Majaji watatu, wakiongozwa na Jaji Dustan Nduguru akisaidiana na Jaji James Karayemaha na Ferdinand Kiwonde.

Tayari Lissu amekamilisha mawasilisho ya mapingamizi yake leo Septemba 11, 2025, madai ya msingi ikiwa ni mchakato wa kesi hiyo katika Mahakama ya Kisutu ulikuwa na makosa mengi na kutaka kesi ifutwe, aachiwe huru, hivyo kinachosubiriwa ni uamuzi kutoka kwa jopo la Majaji watatu.

Iwapo Mahakama Kuu itakubaliana na hoja za Lissu, kesi hiyo inaweza kufutwa rasmi, endapo hoja zikikataliwa basi itaendelea kusikilizwa kwa mujibu wa taratibu za kisheria.

Akizungumza na waandishi wa habari nje ya mahakama hiyo, Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika amesema wakati dunia itakuwa inaadhimisha Siku ya Demokrasia, kwao itakuwa tofauti kwani watakuwa mahakamani kujua hatma ya kesi ya Mwenyekiti wao.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...