Serikali yaondoa pingamizi shauri la Mpina, kesi kusikilizwa Jumatatu

Na Mwandishi Wetu

MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masijala Kuu Dodoma imepanga kusikiliza kesi ya ACT Wazalendo na Luhanga Mpina dhidi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jumatatu Septemba 8,2025.

Shauri hilo limesikilizwa  leo Septemba 3,2025 kwa njia ya mtandao mbele ya jopo la Majaji watatu, Jaji  Evaristo Longopa, Jaji John Kahyoza na Jaji Abdi Kagomba  ambapo Mahakama imeridhia kesi hiyo isikilizwe  ndani ya siku tano kwa njia ya maandishi , huku Mawakili wa pande zote mbili wakitarajiwa takutana Mahakamani kufanya mjumuisho wa hoja zilizowasilishwa kwa maandishi mahakamani hapo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Mwanasheria  Mkuu wa ACT Wazalendo, upande wa Serikali umeamua kuondoa mapingamizi waliyokuwa wameweka awali kuhusiana na kesi hiyo, hatua ambayo imeongeza urahisishaji wa kusikiliza kesi ya msingi.

Kesi hiyo namba 21692/2025, iliyofunguliwa na Bodi ya Wadhamini wa ACT Wazalendo pamoja na Lugaha Mpina, ikipinga uamuzi wa INEC kumuengua mgombea wao  wa Urais, katika orodha ya wagombea.

spot_img

Latest articles

DC Msando aridhishwa uzalishaji maji Ruvu, atoa maagizo Dawasa

Na Mwandishi Wetu MKUU cmwa Wilaya ya Ubungo (DC), Albert Msando amefanya ziara katika...

Mo ajiondoa Bodi ya Wakurugenzi Simba,  Barbara Gonzalez arejea

Na Mwandishi Wetu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Simba, Mohammed Dewji ‘Mo’, ametangaza  kuachana...

Ninatamani Tume ya Charles Keenja irudi Dar es Salaam

TAIFA lipo katika kampeni za uchaguzi mkuu ambao ni mahususi kusaka madaraka ya dola....

Matumizi ya Nishati Safi kupikia yapata msukumo mpya

Na Mwandishi Wetu, Mwanza MATUMIZI ya nishati safi ya kupikia yamepata msukumo mpya jijini Mwanza...

More like this

DC Msando aridhishwa uzalishaji maji Ruvu, atoa maagizo Dawasa

Na Mwandishi Wetu MKUU cmwa Wilaya ya Ubungo (DC), Albert Msando amefanya ziara katika...

Mo ajiondoa Bodi ya Wakurugenzi Simba,  Barbara Gonzalez arejea

Na Mwandishi Wetu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Simba, Mohammed Dewji ‘Mo’, ametangaza  kuachana...

Ninatamani Tume ya Charles Keenja irudi Dar es Salaam

TAIFA lipo katika kampeni za uchaguzi mkuu ambao ni mahususi kusaka madaraka ya dola....