Mfanyabiashara wa nguo ajinyakulia Gari ya IST kupitia SimBanking ya CRDB

Na Mwandishi Wetu

MKAZI wa Tabata jijini Dar es Salaam, Said Mbaruku, ameibuka mshindi wa gari jipya aina ya IST kupitia kampeni ya kipekee ya Benki ya CRDB inayolenga kuhamasisha matumizi ya huduma za kidijitali, hususan SimBanking.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya zawadi hiyo iliyofanyika jana Tabata Segerea , Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi kutoka CRDB, Steven Adili, alisema kampeni hiyo inalenga kurudisha fadhila kwa wateja wao wanaotumia huduma za benki hiyo kwa njia ya kidijitali. 

Alieleza kuwa mbali na magari aina ya IST yanayotolewa kila mwezi, kuna zawadi nyingine mbalimbali zikiwemo fedha taslimu zaidi ya Sh milioni 200 zinazotolewa kila siku.

“Ili kuingia kwenye droo, ni lazima uwe na akaunti ya CRDB na umejiunga na huduma ya SimBanking. Kila muamala unaoufanya, kama vile kununua umeme, kulipia bili, au kukata tiketi za SGR, unakupa nafasi ya kushinda,” alisema Adili.

Kwa mujibu wa CRDB, droo hiyo itaendelea hadi mwezi Disemba ambapo mshindi wa mwisho atajishindia gari aina ya Harrier Anaconda.

“Tunahamasisha wananchi wote kutumia SimBanking. Huduma hii haijabagua ni kwa wanafunzi, wafanyabiashara, wafanyakazi binafsi na hata watumishi wa umma,” aliongeza Adili.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa kampuni tanzu ya CRDB Insurance, Wilson Mzanva alisema kuwa gari lililokabidhiwa mshindi huyo limewekewa mafuta full tank kama sehemu ya kuonesha thamani ya wateja wa benki hiyo.

“CRDB inatoa huduma zake kupitia matawi zaidi ya 260 pamoja na mawakala zaidi ya 25,000 nchi nzima. Kwa sasa, huduma za SimBanking zinapatikana hata kwa wale wasio na smartphone kupitia USSD (*150*03#), pamoja na kupitia app rasmi ya SimBanking,” alisema.

Said Mbaruku, ambaye ni mfanyabiashara wa duka la nguo, alielezea furaha yake baada ya kupokea taarifa za ushindi wake. 

“Nilishangaa sana nilivyopokea SMS kuwa nimeshinda, lakini nilianza kuamini baada ya kupigiwa simu. Sikutarajia kabisa, nilishinda kwa kununua umeme wa Sh 10,000 tu kupitia SimBanking.”

spot_img

Latest articles

Serikali yatoa maelekezo nane kuimarisha kampuni ambazo ina umiliki hisa chache kuelekea Dira 2050

Na Mwandishi wetu, Arusha SERIKALI imetoa maelekezo nane ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa kampuni...

Uwekezaji wa Shilingi Bilioni 50 Kituo Cha Mpomvu waimarisha upatikanaji wa umeme Kanda ya Ziwa

📌 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yakagua Kituo cha Kupokea...

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

CRDB YAZINDUA KAMPENI YA ‘FAINALI NDIO MPANGO NA TEMBOCARD VISA’

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imezindua kampeni yake mpya ya 'Fainali ndio Mpango...

More like this

Serikali yatoa maelekezo nane kuimarisha kampuni ambazo ina umiliki hisa chache kuelekea Dira 2050

Na Mwandishi wetu, Arusha SERIKALI imetoa maelekezo nane ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa kampuni...

Uwekezaji wa Shilingi Bilioni 50 Kituo Cha Mpomvu waimarisha upatikanaji wa umeme Kanda ya Ziwa

📌 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yakagua Kituo cha Kupokea...

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...