Wanaume wana haki ya kulindwa- IGP Wambura

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Camillus Wambura amesema wanaume nchini wana haki ya kulindwa, kusikilizwa na kupewa heshima ambapo wametakiwa kutumia ofisi za Dawati la Jinsia kuripoti ukatili wanaofanyiwa majumbani.

IGP Wambura amesema hayo wakati akifungua Mradi wa Jengo la ofisi za Dawati la Jinsia na Watoto wilayani Tarime, Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya ambapo jengo pamoja na samani zake limegharimu kiasi cha Sh 300 milioni  ikiwa ni  ufadhiri serikali ya Finland.

Aidha, IGP Wambura amewakumbusha wananchi kuwa, serikali kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali imeweza kuweka mikakati madhubuti katika kukabiliana na vitendo vya ukatili wa kijinsia na unyanyasaji dhidi ya watoto ikiwemo makosa ya ukeketaji ili kuhakikisha kuwa wanaojihusisha na vitendo hivyo wanadhibitiwa kwa kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Pia watendaji wa dawati hilo la jinsia wametakiwa kuhakikisha kuwa, wanatoa huduma zenye viwango kwa wateja au wahanga wa matukio ya ukatili wa kijinsia pamoja na kutafuta ufumbuzi wa kukomesha vitendo vya ukatili kwenye jamii.

spot_img

Latest articles

Waziri Mkuu awapongeza watendaji wa Serikali kutekeleza kwa vitendo maono ya Rais Samia

Na Mwandishi Wetu, Dodoma Waziri mkuu  Kassim Majaliwa amesema kuwa Rais  Samia Suluhu Hassan amekuwa nguzo ya...

Bunge  laridhia marekebisho mpaka wa  Hifadhi ya Nyerere

Na Mwandishi Wetu, Dodoma Bunge limeridhia ombi la Serikali la kumega sehemu ya Hifadhi ya...

Rais Mwinyi awatunuku Kamisheni Maafisa wapya wa Idara  Maalum za SMZ

Na Mwandishi Wetu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, ambaye pia ni...

Tumepata somo, tulitumie kukomesha wasiojulikana

LIPO tumaini. Ndivyo inavyoweza kuelezwa kwamba hata katika kiza cha usiku kuna tumaini la...

More like this

Waziri Mkuu awapongeza watendaji wa Serikali kutekeleza kwa vitendo maono ya Rais Samia

Na Mwandishi Wetu, Dodoma Waziri mkuu  Kassim Majaliwa amesema kuwa Rais  Samia Suluhu Hassan amekuwa nguzo ya...

Bunge  laridhia marekebisho mpaka wa  Hifadhi ya Nyerere

Na Mwandishi Wetu, Dodoma Bunge limeridhia ombi la Serikali la kumega sehemu ya Hifadhi ya...

Rais Mwinyi awatunuku Kamisheni Maafisa wapya wa Idara  Maalum za SMZ

Na Mwandishi Wetu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, ambaye pia ni...