Balozi wa Tanzania UAE awasilisha Hati za Utambulisho

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Lt. Jen. (Mst) Yacoub Hassan Mohamed amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu, Sheikh Mohammed Bin Zayed Al Nahyan katika Ikulu ya nchi hiyo iliyopo Mjini Abu Dhabi.

Akizungumza baada ya kupokea hati hizo, Rais Al Nahyan alimuhakikishia, Balozi Mohamed ushirikiano na Serikali yake katika kutekeleza majukumu yake nchini UAE kwa manufaa ya pande zote mbili.

Kwa upande wake Balozi Mohamed alimuahidi, Rais kuwa atahakikisha Watanzania na Waemirati wananufaika na fursa za kiuchumi zilizopo katika pande zote mbili.

Tanzania na UAE zina fursa nyingi za kushirikiana kiuchumi hususan katika sekta ya nishati ambayo UAE ni miongoni mwa nchi tajiri katika uzalishaji wa mafuta. Tanzania ina eneo kubwa la kilimo hivyo ina soko kubwa la bidhaa za Kilimo na Mifugo ambapo ushirikiano huo utawezesha uzalishaji wa kisasa na kuongeza thamani ya bidhaa.

Bidhaa zenye soko kubwa kwa Tanzania nchini UAE ni mbogamboga, matunda, nyama, korosho, karafuu, chai, karanga, asali, samaki na kahawa.

Pamoja na Umoja wa Falme za Kiarabu ubalozi huo pia unawakilisha nchi za Bahrain, Pakistan na Iran.

spot_img

Latest articles

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

More like this

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...