Rais Mwinyi: SMZ kutoa huduma za afya katika Visiwa vidogo vidogo

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali imedhamiria kumaliza matatizo ya kiafya wanayokabiliana nayo Wananchi wanaoishi katika Visiwa Vidogovidogo kwa kufikishwa katika matibabu kwa wakati ili kupunguza vifo vinavyoweza kuepukika ikiwemo vya akinamama na watoto.

Rais Dkt.Mwinyi ameyasema hayo baada ya kuzindua Boti za kubeba Wagonjwa wakati wa dharura hafla iliofanyika Verde Mtoni , Wilaya ya Mjini , Mkoa wa Mjini Magharibi.

Amesema kuwa, Boti hizo ni sehemu ya uimarishaji wa huduma za dharura na mfumo wa wa Rufaa kwa Wagonjwa wanaotoka kwenye Visiwa wanaopewa Rufaa kutoka Vituo vya Afya kwenda Hospitali za Wilaya, Mkoa na Taifa.

Rais Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa Serikali imeamua kuzipeleka Boti hizo katika maeneo yenye changamoto kubwa zaidi na kwengine kutafanyiwa utaratibu wa Haraka baadae.

Aidha, Dkt. Mwinyi ameishukuru Benki ya Dunia kwa kusaidia gharama za Ununuzi wa Boti Tano ambazo tatu tayari zimekamilika na mbili zitakamilika muda mfupi Ujao.

Naye Waziri wa Afya Nassor Ahmed Mazrui amewahakikishia Wananchi wanaoishi katika Visiwa huduma za ihakika zitakazoanza hivi karibuni na kuwa tayari kuzitumia huduma hizo hususan akina Mama na watoto.Boti hizo zimegharimu takribani Shilingi Bilioni 2 na zimetengenezwa na Kampuni ya QIRO GROUP LIMITED.

spot_img

Latest articles

Mnyama Simba afia kwa Mkapa, Yanga, Azam kicheko

Na Winfrida Mtoi LIGI Kuu Tanzania Bara imeendelea leo Novemba 7, 2025 kwa michezo miwili...

Waziri Aweso aweka kambi Dar kupambana na changamoto upungufu wa maji

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso (Mb) amefanya ziara ya kikazi katika...

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

More like this

Mnyama Simba afia kwa Mkapa, Yanga, Azam kicheko

Na Winfrida Mtoi LIGI Kuu Tanzania Bara imeendelea leo Novemba 7, 2025 kwa michezo miwili...

Waziri Aweso aweka kambi Dar kupambana na changamoto upungufu wa maji

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso (Mb) amefanya ziara ya kikazi katika...

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...