Rais Mwinyi: SMZ kutoa huduma za afya katika Visiwa vidogo vidogo

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali imedhamiria kumaliza matatizo ya kiafya wanayokabiliana nayo Wananchi wanaoishi katika Visiwa Vidogovidogo kwa kufikishwa katika matibabu kwa wakati ili kupunguza vifo vinavyoweza kuepukika ikiwemo vya akinamama na watoto.

Rais Dkt.Mwinyi ameyasema hayo baada ya kuzindua Boti za kubeba Wagonjwa wakati wa dharura hafla iliofanyika Verde Mtoni , Wilaya ya Mjini , Mkoa wa Mjini Magharibi.

Amesema kuwa, Boti hizo ni sehemu ya uimarishaji wa huduma za dharura na mfumo wa wa Rufaa kwa Wagonjwa wanaotoka kwenye Visiwa wanaopewa Rufaa kutoka Vituo vya Afya kwenda Hospitali za Wilaya, Mkoa na Taifa.

Rais Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa Serikali imeamua kuzipeleka Boti hizo katika maeneo yenye changamoto kubwa zaidi na kwengine kutafanyiwa utaratibu wa Haraka baadae.

Aidha, Dkt. Mwinyi ameishukuru Benki ya Dunia kwa kusaidia gharama za Ununuzi wa Boti Tano ambazo tatu tayari zimekamilika na mbili zitakamilika muda mfupi Ujao.

Naye Waziri wa Afya Nassor Ahmed Mazrui amewahakikishia Wananchi wanaoishi katika Visiwa huduma za ihakika zitakazoanza hivi karibuni na kuwa tayari kuzitumia huduma hizo hususan akina Mama na watoto.Boti hizo zimegharimu takribani Shilingi Bilioni 2 na zimetengenezwa na Kampuni ya QIRO GROUP LIMITED.

spot_img

Latest articles

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...

Spika wa Bunge ateta na Dk. Mwapinga, amhakikishia ushirikiano

Na Mwandishi Wetu Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani...

More like this

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...