Wataalam 2980 wajengewa uwezo kutoa huduma za afya ya akili

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Khamis Hamza Khamis amesema Serikali inaendelea kufanya jitihada mbalimbali za kudhibiti madhara ya mmomonyoko na kupanuka kwa kingo za mito.

Khamis amesema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Bagamoyo Muharami Mkengealiyetaka kujua ni lini Serikali itajenga Kingo za Mto Mpiji wilayani Bagamoyo mkoani Pwani zilizopanuka kutokana na Mvua kubwa na hivyo kuhatarisha nyumba za wananchi wa maeneo hayo.

Amesema jitihada zilizofanywa na Serikali ni pamoja na kuandaa Mwongozo wa Usafishaji wa Mito ili kuondoa mchanga na tope ambapo kikosi kazi kimeundwa kwa ajili ya kushughulikia suala la usafishaji wa mito.

“Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria ya Mazingira sura 191 kifungu cha 57 (2) kimempa Waziri mamlaka ya kutunga kanuni ndogo na mwongozo na tayari kuna hatua zimeanza kuchukuliwa kwa kufanya doria na kuzuia mali au gari litakalokutwa na kupigwa faini,” amesema Khamis.

Pamoja na hatua hiyo, Naibu Waziri Khamis ameongeza kuwa Serikali inaendelea kutoa elimu kwa wananchi ili watambue umuhimu wa kutunza mazingira katika mito.

Aidha, ameeleza kuwa katika kudhibiti athari za mvua, Serikali inatumia njia za asili za kudhibiti mmomonyoko wa kingo za mito kwa kupanda miche 5,000 aina ya michikichi, migomba, miti maji na matete katika kingo za mto katika eneo lenye ukubwa wa ekari 100 katika Kata ya Mabwepande wilayani Kinondoni mkoani Dar e Salaam.

spot_img

Latest articles

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...

Ofisi ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ya Sabasaba kutangaza huduma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ...

More like this

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...