Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Taarifa Limited inayomilikiwa na mfanyabiashara Rostam Aziz imeingia makubaliano ya kununu hisa za Taasisi ya Aga Khan inazomiliki katika kampuni ya Nation Media Group nchini Kenya.
Taarifa iliyotolewa na Taasisi ya Agakhan leo Machi 10, 2026 kutoka Neneva, Uswisi, imesema kuwa kampuni ya Taarifa Limited, imenunua hiza zote asilimia 54.08 inazomiliki katika kampuni ya Nation.
Mchakato wa kukamilisha mauziano hayo umepangwa kuchukua kati ya miezi mitatu au minne, kutoka Mamlaka za Udhibiti za Kenya.
Hatua ya Rostam Aziz kununua hisa hizo unamrejesha tena mfanyabiashara huyo kuwa miongoni mwa wamiliki wakubwa vyombo vya habari Afrika Mashariki.
Kwa hapa nchini vyombo vya habari vilivyopo ni Mwananchi Communication inayochapisha magazeti ya Mwananchi, Mwanasporti na The Citizen.


