Mwili wa Mwanahabari Mkongwe Makaranga waagwa Dar, kuzikwa Mwanza

Na Mwandishi Wetu

WAANDISHI wa Habari, Wahariri, ndugu na jamaa leo Machi 10, 2026, wamejumuika pamoja katika ibada ya kuaga mwili wa Mhariri Mkongwe, Revocatus Makaranga iliyofanyika kwenye Kanisa Katoliki Parokia ya Kimara, Dar es Salaam.

Makaranga ambaye amewahi kufanya kazi na vyombo vya mbalimbali vya habari nchini, alifariki usiku wa kuamkia Machi 5, 2025, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikopelekwa kwa ajili ya matibabu.

Baada ya ibada ya kutoa heshima za mwisho, mwili wa marehemu umesafirishwa kwenda jijini Mwanza kwa ajili ya mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho.

Marehemu ni mmoja wa waandishi na wahariri wakongwe nchini waliotoa mchango mkubwa katika tasnia ya habari, akifanya kazi katika vyombo vya habari vya umma wakati wa mfumo wa chama kimoja na baadaye vyama vingi, pia alifanya kazi katika kampuni binafsi za Mwananchi Communications Ltd (MCL), New Habari Ltd.

Makaranga ni mhitimu wa shahada ya uzamili katika uandishi wa habari kutoka Chuo Kikuu cha Cardiff, Wales, Uingereza.

spot_img

Latest articles

Wanawake TRA Wapongezwa kwa Mchango wa Ukusanyaji Mapato

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu Mwamba, amewapongeza wanawake wa...

Mchungaji Kimaro: Miradi ya Familia Ndio Suluhisho la Ajira kwa Vijana

Na Mwandishi Wetu  MCHUNGAJI wa Kanisa la Kiinjiri Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kijitonyama Dk....

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani: TRA Yakabidhi Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Milioni 40

Na Tatu Mohamed KUELEKEA maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8,...

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

More like this

Wanawake TRA Wapongezwa kwa Mchango wa Ukusanyaji Mapato

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu Mwamba, amewapongeza wanawake wa...

Mchungaji Kimaro: Miradi ya Familia Ndio Suluhisho la Ajira kwa Vijana

Na Mwandishi Wetu  MCHUNGAJI wa Kanisa la Kiinjiri Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kijitonyama Dk....

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani: TRA Yakabidhi Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Milioni 40

Na Tatu Mohamed KUELEKEA maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8,...