Serikali kupitia REA kuzindua miradi mikubwa ya kimkakati

Na Mwandishi Wetu

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatarajia kuzindua Kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme cha Mtera na Kusaini Mikataba ya kutekeleza mradi wa kusambaza umeme kwenye vitongoji 9,009 katika Mikoa yote Tanzania Bara.

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy amesema hayo Jijini Dodoma  leo Januari 15, 2026 katika mkutano maalum na wanahabari alipokuwa akitambulisha matukio hayo mawili yatakayoshuhudiwa na Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi ambaye atakuwa mgeni rasmi.

“Tarehe 16 Januari, 2026 Kituo cha Kupoza Umeme cha Mtera kitazinduliwa rasmi na tarehe 17 Januari, 2026 tutasaini mikataba 30 yenye thamani ya shilingi Trilioni 1.2 kwa ajili ya kutekeleza mradi mkubwa wa kusambaza umeme katika vitongoji zaidi ya 9,000,” amefafanua Mhandishi Saidy

Amebainisha kuwa Kituo cha Mtera kimejengwa kwa gharama ya sh 9.2  bilioni na Serikali ya Tanzania kupitia REA kwa ushirikiano na Serikali za Sweden na Norway.

Aidha, Mhandisi Saidy amesema REA itasaini mikataba 30 na Wakandarasi 21 wazawa na wakandarasi tisa  kutoka nje ya nchi lakini wamesajiliwa nchini kwa ajili ya kutekeleza mradi huo utakaotekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu ndani ya Mikoa yote Tanzania Bara.

Amewataka wananchi kuchangamkia fursa zitakazopatikana wakati wote wa utekelezaji wake ikiwemo ajira, biashara na huduma mbalimbali zitakazohitajika na pia kuhakikisha wanachangamkia kutumia umeme kuzalisha mali na kuboresha huduma za kijamii.

“Tunatekeleza maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan; mradi huu unakwenda kufungua nchi kiuchumi ni wa kipekee na mradi mkubwa kuwahi kutekelezwa na REA kwa viwango vya gharama na idadi ya vitongoji vitakavyofikiwa,” amesema.

spot_img

Latest articles

Serikali yatoa maelekezo nane kuimarisha kampuni ambazo ina umiliki hisa chache kuelekea Dira 2050

Na Mwandishi wetu, Arusha SERIKALI imetoa maelekezo nane ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa kampuni...

Uwekezaji wa Shilingi Bilioni 50 Kituo Cha Mpomvu waimarisha upatikanaji wa umeme Kanda ya Ziwa

📌 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yakagua Kituo cha Kupokea...

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

CRDB YAZINDUA KAMPENI YA ‘FAINALI NDIO MPANGO NA TEMBOCARD VISA’

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imezindua kampeni yake mpya ya 'Fainali ndio Mpango...

More like this

Serikali yatoa maelekezo nane kuimarisha kampuni ambazo ina umiliki hisa chache kuelekea Dira 2050

Na Mwandishi wetu, Arusha SERIKALI imetoa maelekezo nane ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa kampuni...

Uwekezaji wa Shilingi Bilioni 50 Kituo Cha Mpomvu waimarisha upatikanaji wa umeme Kanda ya Ziwa

📌 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yakagua Kituo cha Kupokea...

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...