Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Familia yaondoa vitu nyumbani kwa Polepole

Na Mwandishi Wetu

FAMILIA ya aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, leo Jumanne, Januari 6, 2026, imefika katika nyumba aliyokuwa akiishi eneo la Ununio jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kukusanya mali zake, pamoja na kufanya maombi kwenye nyumba aliyokuwa akiishi.

Ndugu hao wakiongozwa na mama mzazi wa Humphrey Polepole, Mama Anna Marry Polepole na mdogo wake Godfrey Polepole, wamesema wataendelea kumuombea ndugu yao na kuisihi jamii kuendelea kushirikiana na vyombo husika pale taarifa zozote zitakapopatikana

Akizungumza na waandishi wa habari, Mama wa Polepole ameeleza kuwa wamekwenda kutoa vitu katika nyumba hiyo aliyokuwa amepanda mwanaye kwa sababu hakuna anayeweza kulipa kodi.

Amesisitiza kuwa anaomba waliomchukua mtoto wake wamrudishe akiwa mzima  na ikiwa ana makosa aliyofanya  ashtakiwe kama wengine.

Polepole, ambaye aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini alidaiwa kutekwa na watu wasiojulikana miezi mitatu iliyopita na hadi sasa hatima yake ikiwa bado haijulikani rasmi.

spot_img

Latest articles

Mukwala atua Zanzibar, Simba ikiivaa Azam kesho Mapinduzi Cup

Na Winfrida Mtoi WAKATI Simba kitarajia kukabiliana na Azam FC kesho katika mchezo wa nusu...

Serikali yawekeza zaidi ya Sh. Bilioni 280 kuimarisha upatikanaji umeme Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano...

Chongolo akutana na wawekezaji  kutoka China

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Kilimo, Daniel Chongolo, amekutana na wawekezaji kutoka nchini China  na...

Natoa nishani ya uthubutu kwa Kanisa Katoliki 2025

Siyo hulka yangu kujadili masuala ya dini katika chambuzi ninazofanya. Wala, sikusudii kujikita kuibua...

More like this

Mukwala atua Zanzibar, Simba ikiivaa Azam kesho Mapinduzi Cup

Na Winfrida Mtoi WAKATI Simba kitarajia kukabiliana na Azam FC kesho katika mchezo wa nusu...

Serikali yawekeza zaidi ya Sh. Bilioni 280 kuimarisha upatikanaji umeme Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano...

Chongolo akutana na wawekezaji  kutoka China

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Kilimo, Daniel Chongolo, amekutana na wawekezaji kutoka nchini China  na...