Waziri Mkuu atoa sababu yakutotaja idadi vifo vilivyotokea Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema ni muhimu watanzania kutanguliza utu na heshima kwa familia zilizopoteza wapendwa wao, akipinga namna ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakichapisha taarifa au picha mtandaoni kana kwamba vifo ni jambo la kusherehekewa.

Amesema hayo wakati akijibu maswali aliyoulizwa  kwenye mkutano na wahariri wa vyombo vya habari ya kutaka kujua idadi ya vifo vilivyotokea Oktoba 29, 2025  kutokana na maandamano yaliyofanyika na kusababisha vurugu.

“Tunaongelea maisha ya watu, tunaongelea watu waliopoteza wapendwa wao. Mtu amepoteza ndugu yake halafu wewe unaposti kama hafla,” amesema Waziri Mkuu, akionyesha masikitiko yake juu ya tabia ya kutafuta umaarufu kupitia misiba.

“Katika mazingira ambayo mtu amepoteza mpendwa wake mnataka tuanze kuhesabu kama majengo, magari au mafanikio? Mwingine anataja idadi licha ya kwamba hayupo hapa,” ameeleza.

Aidha Dk. Mwigulu ametaja  vitu vilivyoharibiwa  kutokana na vurugu hizo kuwa ni magari 1,642 ya watu binafsi yaliharibiwa, baadhi yakiteketezwa kwa moto, vituo vya mafuta 672 na bodaboda 2,268.

Amesisitiza umuhimu wa kuzingatia utulivu na amani, akibainisha kuwa Watanzania wanapaswa kuepuka fujo zinazoweza kuharibu maisha na ustawi wa kila mmoja.

Ametoa wito kwa Watanzania kuwa makini na makundi ya watu wenye nia ya kuichafua na kuiharibu Tanzania na wakatae kutumiwa kufanya uovu.

“Kila mmoja alibebe jambo hili kwa ukubwa, hawatupendi, wanaangalia rasilimali zetu, nchi yetu sio masikini, kuna watu wanamezea mate rasilimali zetu, ninawahakikishia kuwa tutailinda Tanzania na Rasilimali zake kwa gharama yoyote ile,”

spot_img

Latest articles

Vijana 3,967 waomba uwezeshaji kupitia Go Green na IMBEJU ya CRDB Bank Foundation

Na Mwandishi wetu JUMLA ya vijana 3,967 kutoka maeneo mbalimbali nchini wamewasilisha maombi ya...

RC Kunenge aipongeza Dawasa, awapa jukumu madiwani

Na Mwandishi wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema ushirikishwaji wananchi kwenye...

Serikali yatoa maelekezo nane kuimarisha kampuni ambazo ina umiliki hisa chache kuelekea Dira 2050

Na Mwandishi wetu, Arusha SERIKALI imetoa maelekezo nane ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa kampuni...

Uwekezaji wa Shilingi Bilioni 50 Kituo Cha Mpomvu waimarisha upatikanaji wa umeme Kanda ya Ziwa

📌 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yakagua Kituo cha Kupokea...

More like this

Vijana 3,967 waomba uwezeshaji kupitia Go Green na IMBEJU ya CRDB Bank Foundation

Na Mwandishi wetu JUMLA ya vijana 3,967 kutoka maeneo mbalimbali nchini wamewasilisha maombi ya...

RC Kunenge aipongeza Dawasa, awapa jukumu madiwani

Na Mwandishi wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema ushirikishwaji wananchi kwenye...

Serikali yatoa maelekezo nane kuimarisha kampuni ambazo ina umiliki hisa chache kuelekea Dira 2050

Na Mwandishi wetu, Arusha SERIKALI imetoa maelekezo nane ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa kampuni...