Niffer arudishwa gerezani, 20 kesi ya uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu

Watuhumiwa 20 kati ya 22 waliokuwa wanashtakiwa kwa makosa ya uhaini wameachiwa huru, huku mfanyabiashara wa vipodozi Jenifer Jovin (26) maarufu Niffer na Mika Lucas Chavala kurudishwa rumande.

Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP) amewafutia kesi hiyo ya uchunguzi namba 26388/ 2025 chini ya kifungu namba 92(1) cha Sheria ya Makosa ya Jinai, Sura ya 20 ilivyofanya marejeo mwaka 2023.

Uamuzi wa kuwafutia kesi hiyo kwa washtakiwa 20, umetolewa leo Jumanne, Novemba 25, 2025 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Aaron Lyamuya, baada ya Wakili wa Ssrikali, Titus Aron kuieleza Mahakaka hiyo kuwa DPP hana nia ya kuendelea na mashtaka dhidi ya washtakiwa 20 kati ya washtakiwa 22 wanakabiliwa na kesi hiyo.

Washtakiwa hao walifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Novemba 7, 2025. Kuachiwa huru kwa baadhi ya watuhumiwa kumekuja kutokana na  kauli ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwamba wale waliofuata mkumbo wakati wa vuguvugu za siku ya uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 iangaliwe namna ya kuachiwa.

spot_img

Latest articles

Waziri Mkuu atoa sababu yakutotaja idadi vifo vilivyotokea Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema ni muhimu watanzania kutanguliza utu na...

Dk.Mwigulu aagiza Kanisa Gwajima lifunguliwe

Na Mwandishi Wetu Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba ameagiza kufunguliwa kwa Kanisa la Ufufuo na...

Ndejembi asisitiza ushirikiano kwa viongozi katika utekelezaji wa miradi yenye kipaumbele kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi (Mb), ametoa wito kwa viongozi na...

Naibu Waziri Nishati, akutana na Menejimenti ya Ewura, aitaka kuongeza kasi na ufanisi zaidi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, leo tarehe 24.11.2025 amekutana na...

More like this

Waziri Mkuu atoa sababu yakutotaja idadi vifo vilivyotokea Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema ni muhimu watanzania kutanguliza utu na...

Dk.Mwigulu aagiza Kanisa Gwajima lifunguliwe

Na Mwandishi Wetu Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba ameagiza kufunguliwa kwa Kanisa la Ufufuo na...

Ndejembi asisitiza ushirikiano kwa viongozi katika utekelezaji wa miradi yenye kipaumbele kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi (Mb), ametoa wito kwa viongozi na...