Watuhumiwa 57 wa uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu

Mahakama ya Wilaya ya Ilemela imewaachia huru watuhumiwa 57 kati 61 wa kesi ya uhaini waliokuwa wakishikiliwa kufuatia  maandamano na matukio ya vurugu za baada ya uchaguzi yalitokea kuanzia Oktoba 29, 2025.

Uamuzi wa kufuta mashtaka hayo umetolewa leo Novemba 24,2025 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Stella Kiama, katika Mahakama ya Wilaya ya Ilemela iliyopo kwenye Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki, Buswelu.

Hatua hiyo imetokana na  upande wa mashtaka, kupitia Wakili wa Serikali Mwandamizi, Safi Amani, kuwasilisha ombi la Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) la kutokuwa na nia ya kuendelea na mashtaka dhidi ya watuhumiwa hao waliokuwa wanakabiliwa na tuhuma mbalimbali.

Shauri hilo namba 26641/2025 limeletwa kwa ajili ya kutajwa kwa mara ya pili mahakamani hapo leo ambapo kwa mara ya kwanza lilitajwa Novemba 24, 2025.

Vijana hao ni miongoni mwa wale waliokuwa wamekamatwa na Jeshi la Polisi na baadaye kufikishwa Mahakamani wakidaiwa kuhusika kwa namna moja au nyingine kwenye maandamano yaliyozaa vurugu zilizopelekea uharibifu wa mali, majeruhi na vifo.

spot_img

Latest articles

Naibu Waziri Nishati, akutana na Menejimenti ya Ewura, aitaka kuongeza kasi na ufanisi zaidi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, leo tarehe 24.11.2025 amekutana na...

Simba yaachia pointi tatu kwa Mkapa, Azam nayo mambo magumu

Na Winfrida Mtoi Simba imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufungwa na Petro de Luanda bao...

Serikali yaahidi kushirikiana na wadau kuendeleza mchezo wa kuogelea

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wakuogelea Afrika Mashariki wamekutana kujadili maendeleo ya mchezo huo,...

Ndejembi: Tanesco mmefanya mageuzi makubwa katika huduma ya umeme kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania...

More like this

Naibu Waziri Nishati, akutana na Menejimenti ya Ewura, aitaka kuongeza kasi na ufanisi zaidi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, leo tarehe 24.11.2025 amekutana na...

Simba yaachia pointi tatu kwa Mkapa, Azam nayo mambo magumu

Na Winfrida Mtoi Simba imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufungwa na Petro de Luanda bao...

Serikali yaahidi kushirikiana na wadau kuendeleza mchezo wa kuogelea

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wakuogelea Afrika Mashariki wamekutana kujadili maendeleo ya mchezo huo,...