Naibu Waziri Nishati, akutana na Menejimenti ya Ewura, aitaka kuongeza kasi na ufanisi zaidi

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, leo tarehe 24.11.2025 amekutana na Menejimenti ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), ikiwa ni mara ya kwanza tangu kuteuliwa katika nafasi hiyo hivi karibuni.

Makamba amekutana na viongozi hao kwa lengo la kujadiliana masuala mbalimbali ya utendaji na maboresho ya sekta ya nishati nchini.

Mkutano huo umefanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya EWURA jijini Dodoma.

Aidha, ameipongeza EWURA kwa kazi nzuri katika kusimamia huduma za nishati, na kuitaka Mamlaka hiyo kuongeza kasi, ubunifu na ufanisi.

“Mimi si muumini wa kushindwa, hivyo natoa rai kwenu kujipanga ili kuendana na kasi hiyo, ili muendelee kung’ara katika uendeshaji wa shughuli zenu” alisema.

Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Andilile, aliwasilisha mbele ya Makamba taarifa fupi kuhusu majukumu ya Mamlaka, mafanikio yaliyopatikana, pamoja na maeneo yanayoendelea kuimarishwa.

Dkt. Andilile aliahidi taasisi yake kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yake ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, salama na za uhakika.

spot_img

Latest articles

Watuhumiwa 57 wa uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Wilaya ya Ilemela imewaachia huru watuhumiwa 57 kati 61 wa...

Simba yaachia pointi tatu kwa Mkapa, Azam nayo mambo magumu

Na Winfrida Mtoi Simba imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufungwa na Petro de Luanda bao...

Serikali yaahidi kushirikiana na wadau kuendeleza mchezo wa kuogelea

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wakuogelea Afrika Mashariki wamekutana kujadili maendeleo ya mchezo huo,...

Ndejembi: Tanesco mmefanya mageuzi makubwa katika huduma ya umeme kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania...

More like this

Watuhumiwa 57 wa uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Wilaya ya Ilemela imewaachia huru watuhumiwa 57 kati 61 wa...

Simba yaachia pointi tatu kwa Mkapa, Azam nayo mambo magumu

Na Winfrida Mtoi Simba imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufungwa na Petro de Luanda bao...

Serikali yaahidi kushirikiana na wadau kuendeleza mchezo wa kuogelea

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wakuogelea Afrika Mashariki wamekutana kujadili maendeleo ya mchezo huo,...