Dk.Mwigulu aagiza Kanisa Gwajima lifunguliwe

Na Mwandishi Wetu

Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba ameagiza kufunguliwa kwa Kanisa la Ufufuo na Uzima, huku akielekeza lipewe miezi sita ya uangalizi katika kuzingatia miiko, masharti na sheria za uendeshwaji wake.

Waziri Dk. Mwigulu amesema hayo wakati akizungumza na wakazi wa Kimara na Mbezi Luis Jijini Dar es Salaam leo November 24, 2025 akiwa katika ziara ya kukagua uharibifu uliotokea katika kipindi cha maandamano na vurugu zilioanza Oktoba 29, 2025 siku ya uchaguzi mkuu.

Ameelekeza kurekebishwa kwa sharti linalotaka kufungiwa kwa nyumba ya ibada iwapo atakosea kiongozi, akisisitiza anayekosea ndiye aadhibiwe bila kuathiri waumini kufanya ibada.

“Natambua ilikuwepo hii moja ya Ufufuo na Uzima kaifungulie, ifungulie wape masharti ya uangalizi ndani ya miezi sita. Ziandikie taasisi zote za kidini kuzikumbusha miiko na mipaka ya ufanyaji kazi, sawa sawa na sheria na Katiba ya nchi yetu.

“Rais Samia ametoa msamaha kwenye Taasisi za kidini ambazo zilikuwa na msukosuko wa hapa na pale, Mh. Waziri wa Mambo ya ndani upo hapa, baada ya hapa fuatilia utaratibu mzuri ziandikie upya Tasisi za kidini, miiko yao, masharti yao ya uandikishwaji yanafikia wapi na zile ambazo zilikuwa na shida shida wape uangalizi wa miesi sita,” ameagiza Dk. Mwigulu.

Kanisa hilo lilikuwa chini ya Josephap Gwajima, lilifutiwa usajili, Juni 2, 2025 kutoka na kukiuka masharti ya uendeshaji wake, kwa kuhusisha siasa ndani yake.

spot_img

Latest articles

Ndejembi asisitiza ushirikiano kwa viongozi katika utekelezaji wa miradi yenye kipaumbele kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi (Mb), ametoa wito kwa viongozi na...

Naibu Waziri Nishati, akutana na Menejimenti ya Ewura, aitaka kuongeza kasi na ufanisi zaidi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, leo tarehe 24.11.2025 amekutana na...

Watuhumiwa 57 wa uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Wilaya ya Ilemela imewaachia huru watuhumiwa 57 kati 61 wa...

Simba yaachia pointi tatu kwa Mkapa, Azam nayo mambo magumu

Na Winfrida Mtoi Simba imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufungwa na Petro de Luanda bao...

More like this

Ndejembi asisitiza ushirikiano kwa viongozi katika utekelezaji wa miradi yenye kipaumbele kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi (Mb), ametoa wito kwa viongozi na...

Naibu Waziri Nishati, akutana na Menejimenti ya Ewura, aitaka kuongeza kasi na ufanisi zaidi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, leo tarehe 24.11.2025 amekutana na...

Watuhumiwa 57 wa uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Wilaya ya Ilemela imewaachia huru watuhumiwa 57 kati 61 wa...