Sababu za kiusalama zazuia Lissu kufikishwa mahakamani

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Magereza limeshindwa kumfikisha mahakamani Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, anayekabiliwa na kesi ya uhaini, kutokana na sababu za kiusalama.

Leo Novemba 10, 2025 Lissu alitarajiwa kufikishwa  katika Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam mbele ya jopo la majaji watatu wa Mahakama Kuu, wakiongozwa na Jaji Dunstan Ndunguru, wakisaidiwa na Majaji James Karayemaha na Ferdinand Kiwonde, kwa ajili ya kusikilizwa kwa shahidi wa nne wa upande wa Jamhuri kutoa ushahidi wake dhidi ya kiongozi huyo wa Chadema.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Thawabu Issa, aliieleza mahakama kuwa walifika mahakamani na  kugundua kwamba mshtakiwa hakuwepo, hivyo kufanya  jitihada za kuwasiliana na Mkuu wa Gereza kujua sababu za kutokuwepo kwake.

“Tulipofika hapa tulikuta mshtakiwa hayupo. Tulifanya jitihada za kuwasiliana na Mkuu wa Gereza na tukaelezwa kwamba wameshindwa kumfikisha kwa sababu za kiusalama,” amesema Wakili Issa.

Upande wa Jamhuri uliiomba Mahakama kuhairisha kesi hiyo kwa siku 14, lakini katika maamuzi yake Mahakama kupitia Jaji Danstan Ndunguru ikatoa maelekezo kuwa shauri hilo linaahirishwa hadi Jumatano na si kwa siku 14 kama ilivyoombwa na Jamhuri. Huku akisisitiza  kuwa mshtakiwa  pamoja na wafikishwe makahamani ili shauri liendelee.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...