Lissu anyimwa dhamana, kesi yaahirishwa hadi Nov 3

Na Mwandishi Wetu

Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu imeahirishwa leo Oktoba 24 hadi Novemba 3, 2025,.

Kesi hiyo iliyoanza kusikilizwa mfululizo tangu Oktoba 6, 2025 imeahirishwa baada ya upande wa Jamhuri kuomba kuahirisha shauri hilo ili kupisha uchaguzi mkuu ambao upo kwa mujibu wa Katiba.

Awali, mshitakiwa Tundu Lissu, aliiomba Mahakama kutoahiriahwa kwa kesi hiyo na kama Mahakama itakubali ombi la upande wa Jamhuri basi yeye apewe dhamana kwa mujibu wa kifungu  302(3) cha Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai (CPA), hadi tarehe iliyopangwa kwenye ratiba ya usikilizaji wa kesi hiyo.

Lissu aliwasilisha ombi hilo leo Ijumaa, Oktoba 24, 2025, mara baada ya Jamhuri kuiomba Mahakama kuahirisha usikilizwaji wa kesi hiyo hadi Novemba 3, 2025, kwa maelezo kuwa mashahidi waliopangwa kutoa ushahidi wao leo wanahusiana na vielelezo vilivyokataliwa wiki hii.

Baada ya kusikiliza ombi la pande zote mbili, Jopo la majaji likiongozwa na Dustan Nduguru limekuja na maamuzi ya kuahirisha kesi hiyo huku wakisema ombi la mshitakiwa kuomba dhamana haliwezekani kwani kesi inayomkabili (Uhaini), haina dhamana.

spot_img

Latest articles

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

Serikali yaahidi kuimarisha uwezeshaji wa Makundi Maalum kupitia ajenda ya Maendeleo Jumuishi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt....

More like this

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...