Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo Kuu la Songea, ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT) – Mwanza, aliyeripotiwa kupotea mnamo Oktoba 09, 2025.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 17,2025  Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Marco  Chilya, amesema Padre huyo hakutekwa kama ambavyo ilidhaniwa bali alijipoteza kutokana na sababu za msongo wa mawazo.

Kamanda huyo ameeleza kuwa Padre amepatikana akiwa hai katika mashamba ya Kijiji cha Mawa, kilichopo Kata ya Hanga, Wilaya ya Namtumbo ambapo ni nyumbani kwao.

Aidha ameongeza kuwa Padre huyo alikutwa akiwa  amedhoofika kwa njaa huku akiwa na begi dogo la mgongoni ambalo lilikuwa na taulo alilokuwa akitumia kulalia, hati yake ya kusafiria, karanga alizokuwa akitumia kama chakula, maji, funguo ya chumba alichokuwa akitumia kabla ya jimboni kwake, fedha taslimu kiasi cha Shilingi 13,500, saa ya mkononi, simu ya mkononi akiwa ameizima  pamoja na dawa za  maumivu.

Ameeleza kuwa  kwa sasa Padre huyo amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songea (Homso) akiendelea na matibabu kutokana na kudhoofika kwa afya yake.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...