Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Matha Japheth (44), kabila ni Mnyamwezi , Mkulima Mkazi wa Kitongoji cha Mzalendo Kijiji cha Mawemeru , Kata ya Nyarugusu Wilaya ya Geita kwa tuhuma za kumuuwa mume wake na kumfukia katika shimo ndani nyumba yao.

Kwa mujibu wa  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Safia Jongo taarifa ya awali inaeleza chanzo ni mgogoro wa kifamilia baina ya mke na mume ambaye kwa sasa ni marehemu.

“Baada ya mahojiano makali mwanamke huyu alikiri kwamba marehemu ni mume wake na kwamba siku hiyo ya tarehe 11 majira ya usiku mwanaume alirudi nyumbani lakini wakawa na ugomvi ambao ulisababisha kumshambulia kwa kitu chenye ncha kali na baada ya kumshambulia mwanaume huyo alifariki dunia na baada ya hapo akaamua kuchimba shimo ndani ya nyumba yao na kisha kumfukia,“ amesema  Kamanda Safia.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...