Rais Samia awapiga chini mabosi Mwendokasi

Na Mwandishi Wetu, The Media Brains

Rais Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa mabosi wapya wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) maarufu Mwendokasi   kwa kuwaondoa Mtendaji  Mkuu Dk. Athuman Kihamia na  Mkurugenzi Mkuu wa kampuni UDART, Waziri Kindamba.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Oktoba 2, 2025 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Sharifa Nyanga, walioteuliwa ni Said Tunda anayechukua nafasi ya Dk. Kihamia na  Pius Ng’ingo anayechukua nafasi ya Waziri Kindamba.

Uteuzi huo unakuja siku moja baada ya wananchi kufanya fujo kwa kupiga mawe mabasi hayo jana katika maeneo ya Magomeni jijini Dar es Salaam kutokana na kuchoshwa na hali ya usafiri  huo.

Wakati uteuzi huo unafanyika tayari mabasi mapya yameanza kufanya kazi katika njia  ya Kimara, Gerezani,  Kivukoni na Morocco.

spot_img

Latest articles

TRA yakusanya Trilioni 8.97 kwa robo ya kwanza, yazidi lengo kwa asilimia 106.3

Na Mwandishi Wetu  MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imetangaza mafanikio ya makusanyo ya mapato kwa...

Kiti Baraza la Usalama kitaondoa maafa Afrika?

MKUTANO Mkuu wa Baraza la Umoja wa Mataifa wa 80 ulimalizika jijini New York,...

Jamii yatakiwa kupaza sauti kukomesha ukatili wa kijinsia

Na Tatu Mohamed JAMII imetakiwa kuendelea kupaza sauti kwa pamoja ili kutokomeza ukatili wa kijinsia...

Bei za Petroli, Dizeli zaendelea kushuka

Na Mwandishi Wetu BEI ya mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa kwa...

More like this

TRA yakusanya Trilioni 8.97 kwa robo ya kwanza, yazidi lengo kwa asilimia 106.3

Na Mwandishi Wetu  MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imetangaza mafanikio ya makusanyo ya mapato kwa...

Kiti Baraza la Usalama kitaondoa maafa Afrika?

MKUTANO Mkuu wa Baraza la Umoja wa Mataifa wa 80 ulimalizika jijini New York,...

Jamii yatakiwa kupaza sauti kukomesha ukatili wa kijinsia

Na Tatu Mohamed JAMII imetakiwa kuendelea kupaza sauti kwa pamoja ili kutokomeza ukatili wa kijinsia...