Na Mwandishi Wetu
TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), imewaasa waandishi wa habari nchini, kujiepusha kuchapisha, kutangaza habari zenye lengo la kuchochea vurugu, ubaguzi, chuki za kisiasa, kikabila, kidini na jinsi.
Hayo yamesemwa na Katibu Mtendaji wa THBUB, Patience Ntwina,, wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari yaliyofanyika leo Jumatatu Septemba 22, 2025 katika Ukumbi wa Tume hiyo, Luthul, Dar es Salaam.
Katika mafunzo hayo yaliyoandaliwa kuhusu Haki za Binadamu na Wajibu wa Waandishi wa Habari wakati wa uchaguzi, Ntwina, alisema kipindi cha kupiga kura katika Uchaguzi MKuu wa Urais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu, waandishi wa habari wanatakiwa kuepuka kufanya kampeni kwa namna yoyote.
Nkwina alisema siku ya kupiga kura haitakiwi kuvaa mavazi yenye alama ya chama au mgombea fulani. Ametoa with kwa waandishi wa habari kuchukua tahadhari dhidi ya matumizi ya mabaya ya majukwaa ya habari ikiwamo mitandao ya kijamii.
Pia amevitaka vyombo vya habari kujikita katika kuimarisha amani, utulivu na demokrasia nchini kwa kutotumika vibaya kalamu zao.