TARURA kushirikiana na Kampuni ya Sukari Kilombero kufanya matengenezo ya Barabara

Na Mwandishi Wetu

WAKALA wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwa kushirikiana na Kampuni ya Sukari ya Kilombero (KSC) wamekubaliana kuanzisha Mfuko wa Barabara kwa ajili ya matengenezo ya barabara kuu za usafirishaji ndani ya wilaya za Kilosa na Kilombero mkoani Morogoro zenye urefu wa Km 206.

Utekelezaji wa mpango huo unatarajiwa kuanza mwaka wa fedha 2025/26 ambapo fedha hizo zitatumika kulipia huduma za matengenezo na ukarabati wa barabara za umma zilizo nje ya mashamba ya Kilombero kwa ajili ya kusafirisha miwa kwenda viwandani K1, K2 na K4.

Kamati ya Mfuko wa Barabara imeweka kipaumbele kwa kazi za awali za matengenezo kwenye barabara zilizotengwa za usafirishaji ndani ya wilaya za Kilosa na Kilombero ambapo barabara zilizotambuliwa kwa ajili ya matengenezo ni sehemu ya mtandao mkuu wa barabara za usafirishaji na zinajumuisha barabara zinazosimamiwa na TARURA.

Jumla ya Kilomita 206 za barabara zitafanyiwa matengenezo, ikiwa kilomita 124.90 ni kwa barabara za wilaya ya Kilombero na kilomita 81.70 kwa barabara za wilaya ya Kilosa. Lengo kuu la mpango huo ni kuziboresha barabara hizo kwani hatua hiyo ni muhimu ili kuhakikisha usafirishaji wa miwa hadi viwandani na pia kusaidia jamii zinazozunguka maeneo hayo.

Mkandarasi atakayehusika na utekelezaji wa kazi hizo ni UNITRANS Tanzania Ltd.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...