Fahad Soud ajinyakulia IST kupitia Simbanking ya CRDB

Na Mwandishi Wetu

MKAZI wa Jiji la Tanga, Fahad Soud, ameibuka mshindi wa pili wa gari jipya aina ya IST kupitia kampeni ya Benki ya CRDB inayolenga kuhamasisha matumizi ya huduma za kidijitali, hususan SimBanking.

Hafla ya makabidhiano ya zawadi hiyo ilifanyika jana katika Viwanja vya Dar Village, Mikocheni jijini Dar es Salaam ambapo ilihudhuriwa na viongozi waandamizi wa benki hiyo na wadau mbalimbali.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa CRDB, Stephen Adili, alisema kampeni hiyo ni sehemu ya kurudisha fadhila kwa wateja wanaotumia huduma za kidijitali za benki hiyo.

“Mbali na magari aina ya IST yanayotolewa kila mwezi, zawadi nyingine mbalimbali kama fedha taslimu pia zinapatikana. Ili kushiriki, mteja anatakiwa kuwa na akaunti ya CRDB na amejiunga na SimBanking. Kila muamala unakupa nafasi ya kushinda, iwe ni kununua umeme, kulipia bili au kukata tiketi za SGR,” alisema Adili.

Kwa mujibu wa CRDB, droo hiyo itaendelea hadi mwezi Disemba ambapo mshindi wa mwisho atajinyakulia gari aina ya Harrier Anaconda, huku wateja wengine wakiendelea kujipatia zawadi mbalimbali kila mwezi.

Adili alisisitiza kuwa huduma ya SimBanking ni jumuishi na haina mipaka kwa kundi maalumu la wateja, kwani inawahusu wanafunzi, wafanyabiashara, watumishi wa umma na hata wafanyakazi binafsi.

Kwa upande wake, mshindi wa zawadi hiyo, Fahad Soud, aliishukuru Benki ya CRDB kwa kuendesha kampeni hiyo na kuwataka wateja wengine kujitokeza kwa wingi kutumia SimBanking.

“Nimefurahi sana kushinda gari kupitia huduma hii. Naomba Watanzania waamini kwamba kampeni hii ni ya kweli na washiriki kwa kufanya miamala kupitia SimBanking ili nao waweze kushinda kama mimi,” alisema Fahad.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...