Mkurugenzi Mkuu Dawasa Mtaa kwa Mtaa kukagua huduma za maji

Na Mwandishi Wetu

AFISA Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Mkama Bwire amefanya ziara ya kikazi kukagua hali ya upatikanaji wa maji katika maeneo ya Ubungo, Mburahati, Magomeni, Saranga na Kinyerezi.

Ziara hiyo ililenga kujionea hali halisi ya upatikanaji wa maji na kutafuta suluhisho katika maeneo yenye changamoto za kihuduma zinazowakabili wananchi.

“Huduma ya Maji katika eneo letu la kihuduma Dar na Pwani iko vizuri na leo tunapita mitaani kukagua na kujiridhisha upatikanaji wa huduma tunayozalisha kama inawafikia wananchi na iwapo kama kuna changamoto basi tunazitatua na wananchi wanaendelea kufurahia huduma” amesema Mhandisi Bwire.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mtaa wa Kinyerezi, Hassan Hamiss Nandeta, ameishukuru DAWASA kwa hatua madhubuti ilizochukua katika kuboresha huduma ya maji safi kwenye maeneo yao, akibainisha kuwa wananchi wameanza kunufaika na maboresho hayo.

DAWASA inaendelea kutekeleza mkakati wa kuboresha huduma za maji safi na usafi wa mazingira kwa wakazi wa Dar es Salaam na maeneo jirani, ikiwa ni sehemu ya dhamira yake ya kuhakikisha kila mteja anapata huduma bora na ya uhakika.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...