Ajali yaua wanafunzi wawili wa kidato cha sita

Na Mwandishi Wetu

Watu saba wamefariki dunia wakiwamo wanafunzi wawili wa kidato cha sita shule ya Sekondari Songe, Musoma baada ya gari aina ya Toyota Succeed walilokuwa wakisafiria kugonga kwa nyuma Fuso lililokuwa limeegeshwa barabarani baada ya kuharibika.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Tarime/Rorya, Mark Njera, ajali hiyo imetokea Kijiji cha Buganjo wilayani Rorya leo Septemba 11,2025 saa 11 alfajiri.

Amewataja wanafunzi hao kuwa ni Kwinta Gerald(18) Anitha Selemani(18). Wengine waliofariki ni Kelivin Orando(28), Ombura Ududo(34), John Abraham(30), Sharome Benard(30) wote wakazi wa Rorya.

Kamanda Njera amesema uchunguzi wa awali umebaini chanzo cha ajali hiyo ni  ni mwendokasi wa dereva wa gari aina ya Toyota Succeed kwa kuendesha bila kuchukua tahadhari.

Ameeleza kuwa dereva wa gari aina ya Mitsubish Fuso iliyokuwa  imeharibika na kupaki pembeni  mwa barabara ilichukua tahadhari  kwa kuweka  alama(reflective triangle).

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...