Ajali yaua wanafunzi wawili wa kidato cha sita

Na Mwandishi Wetu

Watu saba wamefariki dunia wakiwamo wanafunzi wawili wa kidato cha sita shule ya Sekondari Songe, Musoma baada ya gari aina ya Toyota Succeed walilokuwa wakisafiria kugonga kwa nyuma Fuso lililokuwa limeegeshwa barabarani baada ya kuharibika.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Tarime/Rorya, Mark Njera, ajali hiyo imetokea Kijiji cha Buganjo wilayani Rorya leo Septemba 11,2025 saa 11 alfajiri.

Amewataja wanafunzi hao kuwa ni Kwinta Gerald(18) Anitha Selemani(18). Wengine waliofariki ni Kelivin Orando(28), Ombura Ududo(34), John Abraham(30), Sharome Benard(30) wote wakazi wa Rorya.

Kamanda Njera amesema uchunguzi wa awali umebaini chanzo cha ajali hiyo ni  ni mwendokasi wa dereva wa gari aina ya Toyota Succeed kwa kuendesha bila kuchukua tahadhari.

Ameeleza kuwa dereva wa gari aina ya Mitsubish Fuso iliyokuwa  imeharibika na kupaki pembeni  mwa barabara ilichukua tahadhari  kwa kuweka  alama(reflective triangle).

spot_img

Latest articles

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

Serikali yaahidi kuimarisha uwezeshaji wa Makundi Maalum kupitia ajenda ya Maendeleo Jumuishi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt....

More like this

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...