INEC yatoa wito kwa asasi za kiraia

Na Mwandishi Wetu

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imezitaka taasisi na asasi za kiraia zilizopata kibali cha kutoa elimu ya mpiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kutekeleza jukumu hilo kwa ufanisi na weledi.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa INEC, Kailima Ramadhani, ametoa wito huo leo Septemba 8, 2025, wakati wa kufungua kikao kazi kati ya Tume na taasisi pamoja na asasi hizo kilichofanyika mkoani Dodoma.

Kailima ameongeza kuwa INEC inatarajia kuona taasisi na asasi za kiraia zikitoa elimu iliyolengwa, huku zikisisitiza masuala yanayowapa wananchi, wagombea, na vyama vya siasa uelewa juu ya kushiriki katika kampeni kwa amani na utulivu, ikiwa ni pamoja na kuelewa vyema utaratibu wa kupiga kura.

“Hatutegemei kabisa mtatoa elimu itakayoichanganya jamii na kuipeleka nchi katika machafuko, kama ilivyoshuhudiwa katika baadhi ya maeneo Afrika na duniani kwa ujumla,” amesema Kailima.

Amesisitiza kuwa taasisi na asasi hizo haziruhusiwi kuwapa watu wengine, taasisi au asasi vibali walivyopewa, na kwamba vibali hivyo vinapaswa kutumiwa na walengwa pekee.

Kikao kazi hicho kimewahusisha viongozi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na wawakilishi wa taasisi na asasi 164 zilizopewa vibali vya kutoa elimu ya mpiga kura ambapo mada mbalimbali zimewasilishwa.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...