Serikali yaondoa pingamizi shauri la Mpina, kesi kusikilizwa Jumatatu

Na Mwandishi Wetu

MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masijala Kuu Dodoma imepanga kusikiliza kesi ya ACT Wazalendo na Luhanga Mpina dhidi ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jumatatu Septemba 8,2025.

Shauri hilo limesikilizwa  leo Septemba 3,2025 kwa njia ya mtandao mbele ya jopo la Majaji watatu, Jaji  Evaristo Longopa, Jaji John Kahyoza na Jaji Abdi Kagomba  ambapo Mahakama imeridhia kesi hiyo isikilizwe  ndani ya siku tano kwa njia ya maandishi , huku Mawakili wa pande zote mbili wakitarajiwa takutana Mahakamani kufanya mjumuisho wa hoja zilizowasilishwa kwa maandishi mahakamani hapo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Mwanasheria  Mkuu wa ACT Wazalendo, upande wa Serikali umeamua kuondoa mapingamizi waliyokuwa wameweka awali kuhusiana na kesi hiyo, hatua ambayo imeongeza urahisishaji wa kusikiliza kesi ya msingi.

Kesi hiyo namba 21692/2025, iliyofunguliwa na Bodi ya Wadhamini wa ACT Wazalendo pamoja na Lugaha Mpina, ikipinga uamuzi wa INEC kumuengua mgombea wao  wa Urais, katika orodha ya wagombea.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...