Jeshi la Polisi  lakabidhiwa mashine ya kuweka silaha alama

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi nchini limekabidhiwa mashine maalumu ya kuweka alama silaha zilizopo nchini ikiwa ni hatua mbalimbali zinazochukuliwa katika kuzuia uzagaaji wa silaha ndogondogo na nyepesi ili kuepuka madhara yanayoweza kuwapata wananchi na nchi kwa ujumla.

Mashine hizo mbili zimekabidhiwa na Mwakilishi wa Taasisi ya Kikanda ya kupambana na uzagaaji wa silaha haramu na nyepesi katika Ukanda wa Maziwa Makuu na Pembe ya Afrika (RECSA), Eric Kailanga na kupokelewa na Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Zanzibar, DCP Zuberi Chembera wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya uwekaji alama na kutunza kumbukumbu za silaha kwa Askari Polisi jijini Dodoma.

Akizungumza baada ya kupokea mashine hizo, DCP Chembera amesema Jeshi la Polisi limeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuhakikisha kuwa nchi yetu inaendelea kuwa salama na kupatikana kwa mashine hizo kutasaidia kwa kiasi kikubwa juhudi hizo.

Aidha, aliwataka washiriki wa mafunzo ya uwekaji alama kuzingatia kikamilifu mafunzo watakayopata ili kuhakikisha kuwa utendaji wao unazidi kuimarika na kwenda kuwafundisha wengine ambao hawajapata fursa hiyo.

Kwa upande wake Mratibu wa Kitaifa wa Udhibiti wa Silaha ndogondogo na nyepesi nchini, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Berthaneema Mlay amesema mashine hizo mpya walizopatiwa ni za kisasa na zitaendelea kuimarisha utendaji kazi wa kudhibiti silaha haramu nchini.

Naye Mwakilishi wa kituo cha RECSA, Eric Kayiranga amesema kituo hicho kitaendelea kushirikiana na nchi wanachama katika kuhakikisha kuwa mafunzo ya mara kwa mara yanafanyika kwa lengo la kuongeza weledi kwa vyombo na taasisi zinazosimamia sheria.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...