VETA Kihonda yabuni mashine ya kusaga chumvi, kuinua thamani ya zao hilo

Na Tatu Mohamed, Dodoma

CHUO cha VETA Kihonda kimebuni mashine mpya ya kusaga chumvi ya mawe, hatua inayolenga kuongeza thamani ya zao hilo na kurahisisha matumizi yake katika sekta mbalimbali.

Akizungumza kwenye Maonesho ya Wakulima na Wafugaji (Nanenane) yanayofanyika kitaifa jijini Dodoma, Mkufunzi Mwandamizi wa chuo hicho, Fredrick Uliki, amesema mashine hiyo imeundwa mahsusi kwa ajili ya kusaidia wakulima wadogo wa chumvi hususani wa Bagamoyo na Lindi ambao wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya kusaga chumvi.

“Chumvi inapokuwa unga, matumizi yake yanapanuka zaidi. Kwa mfano, kwenye nyama ya kuchoma au chakula cha mifugo, ni lazima utumie chumvi ya unga. Pia, chumvi ikisagwa ni rahisi kuongeza madini joto na virutubishi vingine,” amesema Uliki.

Amefafanua kuwa, Mashine hiyo ina uwezo wa kusaga kilo 100 hadi 150 kwa saa, na imetengenezwa kwa malighafi imara zisizoshika kutu, jambo linaloifanya idumu kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa Uliki, teknolojia hiyo inalenga kusaidia wakulima kuongeza thamani ya chumvi yao, kuisafirisha kwa urahisi zaidi na kupata soko pana.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...