VETA Kihonda yabuni mashine ya kusaga chumvi, kuinua thamani ya zao hilo

Na Tatu Mohamed, Dodoma

CHUO cha VETA Kihonda kimebuni mashine mpya ya kusaga chumvi ya mawe, hatua inayolenga kuongeza thamani ya zao hilo na kurahisisha matumizi yake katika sekta mbalimbali.

Akizungumza kwenye Maonesho ya Wakulima na Wafugaji (Nanenane) yanayofanyika kitaifa jijini Dodoma, Mkufunzi Mwandamizi wa chuo hicho, Fredrick Uliki, amesema mashine hiyo imeundwa mahsusi kwa ajili ya kusaidia wakulima wadogo wa chumvi hususani wa Bagamoyo na Lindi ambao wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya kusaga chumvi.

“Chumvi inapokuwa unga, matumizi yake yanapanuka zaidi. Kwa mfano, kwenye nyama ya kuchoma au chakula cha mifugo, ni lazima utumie chumvi ya unga. Pia, chumvi ikisagwa ni rahisi kuongeza madini joto na virutubishi vingine,” amesema Uliki.

Amefafanua kuwa, Mashine hiyo ina uwezo wa kusaga kilo 100 hadi 150 kwa saa, na imetengenezwa kwa malighafi imara zisizoshika kutu, jambo linaloifanya idumu kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa Uliki, teknolojia hiyo inalenga kusaidia wakulima kuongeza thamani ya chumvi yao, kuisafirisha kwa urahisi zaidi na kupata soko pana.

spot_img

Latest articles

Jeuri ya ushindi CAFCL Simba waanza ‘kuchonga’

Na Winfrida Mtoi Ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nsingizini Hotspurs katika mchezo wa Ligi ya...

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

More like this

Jeuri ya ushindi CAFCL Simba waanza ‘kuchonga’

Na Winfrida Mtoi Ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nsingizini Hotspurs katika mchezo wa Ligi ya...

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...