Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora yaweka wazi nafasi yake kwenye Uchaguzi Mkuu

Na Tatu Mohamed

TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imesema kuwa ina wajibu kuhakikisha Uchaguzi Mkuu unakuwa huru na wa haki nchini.

Hayo yameelezwa na Kamishna Mkazi wa Tume Zanzibar, Khatib Mwinyichande, wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye banda lao lililopo katika Viwanja vya Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (Sabasaba) yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere.

Alisema Sabasaba ni fursa muhimu ya kuwa karibu na wananchi, kupokea malalamiko yao, na kuwaelimisha kuhusu haki zao za msingi.

“Maonyesho haya yanatupa nafasi ya kukutana moja kwa moja na wananchi. Tunalinda haki zao, tunawaelimisha kuhusu wajibu wao, na tunawakumbusha kuwa hakuna mtu anayepaswa kunyimwa haki yake kwa misingi yoyote,” alisema Kamishna Mwinyichande.

Aidha, alieleza kuwa Tume hiyo, kama chombo huru cha kikatiba, ina wajibu wa kuhakikisha uchaguzi mkuu nchini unakuwa huru, wa haki na unaozingatia misingi ya utawala bora.

“Uchaguzi si tukio la kisiasa tu, bali ni haki ya msingi kwa wananchi. Tume yetu ina jukumu la kuhakikisha kuwa mchakato wote wa uchaguzi unazingatia sheria, haki za binadamu na misingi ya demokrasia,” alibainisha.

Mwinyichande alisema Tume itakuwa miongoni mwa waangalizi wa uchaguzi mkuu, kuanzia kampeni hadi upigaji kura, na itakuwa ikifuatilia mwenendo wa uchaguzi ili kubaini changamoto na mapungufu yanayoweza kuathiri haki za wananchi, kisha kuwasilisha ripoti kwa mamlaka husika kwa ajili ya maboresho ya baadaye.

Alisisitiza kuwa kazi ya Tume si tu kulinda haki baada ya matatizo kutokea, bali pia ni kuzuia ukiukwaji wa haki kabla haujatokea kwa njia ya elimu na ushawishi wa sera zenye mwelekeo wa haki na usawa.

Kwa ujumla, ushiriki wa Tume ya Haki za Binadamu katika Sabasaba mwaka huu umeonesha namna taasisi za umma zinavyoweza kutumia majukwaa ya kijamii kuimarisha uelewa wa wananchi kuhusu haki zao, wajibu wao, na njia salama za kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi kupitia uchaguzi wa kidemokrasia.

spot_img

Latest articles

TMDA yaendelea kuelimisha umma juu ya matumizi sahihi ya dawa Sabasaba

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), Imeendelea kutoa Elimu kwa...

Mazingira wezeshi ya Serikali yafungua fursa mpya za Uwekezaji kupitia TAWA

📍 Milango ya uwekezaji bado iko wazi Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usimamizi wa...

CRDB yamkabidhi Rahabu Mwambene zawadi ya gari aina ya Ford Ranger XLT 

Na Mwandishi Wetu  BENKI ya CRDB imemkabidhi Rahabu Mwambene zawadi ya gari aina ya Ford...

Baba Levo atembelea Banda la TTCL Sabasaba, apongeza Mapinduzi ya Kidijitali

Na Mwandishi Wetu MSANII na mtangazaji maarufu nchini, Clayton Chipando maarufu kama Baba Levo,...

More like this

TMDA yaendelea kuelimisha umma juu ya matumizi sahihi ya dawa Sabasaba

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), Imeendelea kutoa Elimu kwa...

Mazingira wezeshi ya Serikali yafungua fursa mpya za Uwekezaji kupitia TAWA

📍 Milango ya uwekezaji bado iko wazi Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usimamizi wa...

CRDB yamkabidhi Rahabu Mwambene zawadi ya gari aina ya Ford Ranger XLT 

Na Mwandishi Wetu  BENKI ya CRDB imemkabidhi Rahabu Mwambene zawadi ya gari aina ya Ford...