Waziri Mkuu awapongeza watendaji wa Serikali kutekeleza kwa vitendo maono ya Rais Samia

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Waziri mkuu  Kassim Majaliwa amesema kuwa Rais  Samia Suluhu Hassan amekuwa nguzo ya kuimarisha mshikamano na umoja wa kitaifa na kufanikisha maendeleo katika sekta mbalimbali za maendeleo.

Amesema kuwa katika kipindi cha uongozi wake, Rais ameweza kusimama imara katika kuendeleza miradi ya kimkakati na huduma za jamii, kusimamia demokrasia, kujenga uchumi na kuimarisha diplomasia.

Amesema hayo leo Juni 26, 2025, wakati alipotoa hoja ya kukamilisha shughuli za Bunge la 12, Bungeni jijini Dodoma.

“Sina shaka nyote mtakubaliana nami kuwa hulka yake na ustahimilivu wake umekuwa faraja kwetu sisi wasaidizi wake, watumishi wote wa umma na Watanzania wote kwa ujumla. Isitoshe, Mheshimiwa Rais wakati wote amekuwa nguzo ya kuimarisha mshikamano na umoja wa kitaifa,”

Amesema  Rais Samia amekuwa mwalimu wa subira, kielelezo cha ujasiri, ustahimilivu na alama ya matumaini kwa kizazi hiki. “Ni kiongozi aliyetoa mfano wa kuwa mwanamke anaweza kuongoza hata kwenye nafasi ya Kitaifa.”

Majaliwa amesema kuwa kutokana na uongozi dhabiti wa Rais Samia, taasisi mbalimbali za kitaifa na kimataifa zimetambua mchango na maono yake katika kusimamia shughuli za kimaendeleo nchini na kuitangaza Tanzania nje ya nchi.

Ametaja tuzo za kimataifa  alizopokea   Rais kuwa  ni Global Gates Goalkeepers, Tuzo ya Babacar Ndiaye kwa mwaka 2022, Tuzo ya Uongozi wa Kimageuzi Afrika, Tuzo ya Heshima ya Pyne Africa Awards 2022 na Tuzo ya Muongoza Watalii Bora.

Tuzo nyingine alizopata kitaifa ni Tuzo Maalum ya Heshima ya kutambua mchango wake katika kulitumikia Taifa na kuwaletea wananchi maendeleo iliyotolewa na Bunge, Tuzo Maalum ya kutambua dhamira yake thabiti ya kujenga Taifa linalostahimili Mabadiliko ya Tabianchi.

spot_img

Latest articles

Bunge  laridhia marekebisho mpaka wa  Hifadhi ya Nyerere

Na Mwandishi Wetu, Dodoma Bunge limeridhia ombi la Serikali la kumega sehemu ya Hifadhi ya...

Rais Mwinyi awatunuku Kamisheni Maafisa wapya wa Idara  Maalum za SMZ

Na Mwandishi Wetu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, ambaye pia ni...

Tumepata somo, tulitumie kukomesha wasiojulikana

LIPO tumaini. Ndivyo inavyoweza kuelezwa kwamba hata katika kiza cha usiku kuna tumaini la...

Yanga Bingwa Ligi Kuu msimu wa 2024/25

Na Mwandishi Wetu Yanga imefanikiwa kutetea ubingwa wake wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kuichapa...

More like this

Bunge  laridhia marekebisho mpaka wa  Hifadhi ya Nyerere

Na Mwandishi Wetu, Dodoma Bunge limeridhia ombi la Serikali la kumega sehemu ya Hifadhi ya...

Rais Mwinyi awatunuku Kamisheni Maafisa wapya wa Idara  Maalum za SMZ

Na Mwandishi Wetu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, ambaye pia ni...

Tumepata somo, tulitumie kukomesha wasiojulikana

LIPO tumaini. Ndivyo inavyoweza kuelezwa kwamba hata katika kiza cha usiku kuna tumaini la...