Wanaume wana haki ya kulindwa- IGP Wambura

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Camillus Wambura amesema wanaume nchini wana haki ya kulindwa, kusikilizwa na kupewa heshima ambapo wametakiwa kutumia ofisi za Dawati la Jinsia kuripoti ukatili wanaofanyiwa majumbani.

IGP Wambura amesema hayo wakati akifungua Mradi wa Jengo la ofisi za Dawati la Jinsia na Watoto wilayani Tarime, Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya ambapo jengo pamoja na samani zake limegharimu kiasi cha Sh 300 milioni  ikiwa ni  ufadhiri serikali ya Finland.

Aidha, IGP Wambura amewakumbusha wananchi kuwa, serikali kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali imeweza kuweka mikakati madhubuti katika kukabiliana na vitendo vya ukatili wa kijinsia na unyanyasaji dhidi ya watoto ikiwemo makosa ya ukeketaji ili kuhakikisha kuwa wanaojihusisha na vitendo hivyo wanadhibitiwa kwa kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Pia watendaji wa dawati hilo la jinsia wametakiwa kuhakikisha kuwa, wanatoa huduma zenye viwango kwa wateja au wahanga wa matukio ya ukatili wa kijinsia pamoja na kutafuta ufumbuzi wa kukomesha vitendo vya ukatili kwenye jamii.

spot_img

Latest articles

Tumepata somo, tulitumie kukomesha wasiojulikana

LIPO tumaini. Ndivyo inavyoweza kuelezwa kwamba hata katika kiza cha usiku kuna tumaini la...

Yanga Bingwa Ligi Kuu msimu wa 2024/25

Na Mwandishi Wetu Yanga imefanikiwa kutetea ubingwa wake wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kuichapa...

Tanzania, Msumbiji  kuimarisha uhusiano kibiashara 

Na Mwandishi Wetu Rais Samia  Suluhu Hassan, amesema  Tanzania itaendelea kushirikiana na   Msumbiji katika  kuleta maendeleo , ustawi wa...

Malalamiko 461 Yawasilishwa EWURA Kwa Miaka Miwili

Na Tatu Mohamed  MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imesema katika...

More like this

Tumepata somo, tulitumie kukomesha wasiojulikana

LIPO tumaini. Ndivyo inavyoweza kuelezwa kwamba hata katika kiza cha usiku kuna tumaini la...

Yanga Bingwa Ligi Kuu msimu wa 2024/25

Na Mwandishi Wetu Yanga imefanikiwa kutetea ubingwa wake wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kuichapa...

Tanzania, Msumbiji  kuimarisha uhusiano kibiashara 

Na Mwandishi Wetu Rais Samia  Suluhu Hassan, amesema  Tanzania itaendelea kushirikiana na   Msumbiji katika  kuleta maendeleo , ustawi wa...