Wizara ya Elimu yazindua kituo cha huduma kwa wateja

Na Mwandishi Wetu

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, imezindua Kituo cha Huduma kwa wateja, kilichograimu takribani  Sh 100 milioni kwa lengo la kuanza kupokea ushauri,maoni na mawazo ya watu mbalimbali ili kuhakikisha  wizara hiyo inaendelea kuboresha sekta ya elimu.

Kituo hicho kimefadhiliwa kwa kiasi kikubwa na Serikali ya Uingereza kupitia ofisi yake ya Commonwealth na mradi wa shule bora

Akizungumza jijini Dodoma baada ya kuzindua Kituo hicho Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia,Omari Kipanga, amesema kuwa kupitia kituo hicho anaamini wataweza kushughulikia changamoto mbalimbali ambazo zipo katika Wizara hiyo.

“Kupitia kituo hichi tutaenda kutatua changamoto pamoja na kwenda kufanya kazi kwa weledi lengo letu tunataka wizara yetu izidi kusonga mbele katika masuala ya elimu,”amesema Kipanga.

Aidha amesema kuwa  Serikali kupitia wizara hiyo  iliona ni muhimu kuwa na kituo hicho ili kuanza kupokea ushauri,maoni na mawazo ya watu mbalimbali ili kuhakikisha wanaendelea kuboresha elimu.

“Kipekee niwashukuru na kuipongeza serikali ya Uingereza kwa  kukiboresha kituo hiki kutoka Call Center hadi Contact Center na sisi tunaahidi tutatunza vifaa walivyowezeshwa,” ameeleza.

Hata hivyo amesema kuwa  wafanyakazi wa kituo hicho tayari wameshapata mafunzo na wana amini  watafanyakazi kwa weledi kuhakikisha wanawahudumia watanzania.

Awali Katibu Mkuu  wa Wizara hiyo Prof.  Carolyne Nombo,amesema kuwa kituo hicho wamekisubiri kwa muda wa miaka miwili na  sasa kimekamilika.

“Kupitia kituo hiki tunaenda kuwasiliana na wananchi katika maboresho ya elimu, Wizara  itaenda kutunza kituo hiki na kuhakikisha kwamba huduma ambazo zinatolewa zitakuwa bora na katika miaka ijayo,” amesema Prof.Nombo

Kwa upande wake Mwakilishi wa Ubalozi wa Uingreza Dk.John Lusingu,ametoa wito kwa watendaji wa wizara hiyo kutekeleza maoni ya wananchi.

spot_img

Latest articles

Watanzania  wako tayari kuchangia  harusi, sio gharama za matibabu ya mtoto- Dk. Mollel

Na Mwandishi Wetu Serikali imetoa wito kwa wananchi kubadilika na kuwekeza katika bima ya afya...

Watu tisa wafariki dunia, 44 wajeruhiwa ajali ya basi na Lori Morogoro

Na Mwandishi Wetu Watu tisa wamefariki dunia papo hapo na wengine 44 kujeruhiwa baada ya...

Ndege ya Air India yaanguka, ikiwa na abiria  242

Na Mwandishi Wetu Ndege ya abiria ya Shirika la Ndege la  India ‘Air India’  iliyokuwa inatokea nchini...

Kweli IJP Wambura Polisi wamefanikiwa, sasa umma unataka kujua wasiojulikana

JUMATATU wiki hii Jeshi la Polisi lilikuwa na mahafali ya maofisa wa vyeo vya...

More like this

Watanzania  wako tayari kuchangia  harusi, sio gharama za matibabu ya mtoto- Dk. Mollel

Na Mwandishi Wetu Serikali imetoa wito kwa wananchi kubadilika na kuwekeza katika bima ya afya...

Watu tisa wafariki dunia, 44 wajeruhiwa ajali ya basi na Lori Morogoro

Na Mwandishi Wetu Watu tisa wamefariki dunia papo hapo na wengine 44 kujeruhiwa baada ya...

Ndege ya Air India yaanguka, ikiwa na abiria  242

Na Mwandishi Wetu Ndege ya abiria ya Shirika la Ndege la  India ‘Air India’  iliyokuwa inatokea nchini...